logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sijawahi kuumizwa moyo na mwanamke yeyote maishani mwangu - Jay Melody

Sijawahi kuumizwa na Mapenzi maishani labda mimi ndio nimumize Mtu

image
na

Habari06 May 2024 - 11:51

Muhtasari


•Melody alisema amefanya mambo kadhaa ya kuvunja moyo kwa wanawake lakini hajawahi kuyapitia yeye mwenyewe.

•Sijawahi kuumizwa na Mapenzi maishani labda mimi ndio nimumize Mtu.

Jay Melody.

Melody alisema amefanya mambo kadhaa ya kuvunja moyo kwa wanawake lakini hajawahi kuyapitia yeye mwenyewe

Mwimbaji kutoka Tanzania Jay Melody anayefahamika kwa kuachia nyimbo kibao za mapenzi amefichua kuwa kamwe katika maisha yake hajawahi kuumia moyo kutokana na mapenzi.

Melody alisema amefanya mambo kadhaa ya kuvunja moyo kwa wanawake lakini hajawahi kuyapitia yeye mwenyewe.

“Sijawahi kuumizwa na Mapenzi maishani labda mimi ndio nimumize Mtu.” Alisema 

Alitoa mfano wa mwanamke ambaye alikataa wanaume wengi lakini akamchangua yeye lakini baadae alimkataa.

Jambo kubwa ambalo siwezi kulisahau ni kumkataa mrembo aliyetongozwa na wanaume 16 lakini hakuwataka, alinichagua nikakataa.”

Melody alithibitisha kuwa anachumbiana  “Napenda maisha ya hali ya chini, sipendi kumpost mpenzi wangu, nikifanya hivyo ina maana nafunguka mambo mengi, watu wenye pesa wataanza kumpiga, sipendi maisha yangu. sana kwenye mitandao ya kijamii hadi nashindwa kuiishi."


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved