logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Watoto wauawa wakati bomu likianguka karibu na hospitali ya Sudan

Tangu Ijumaa, wakaazi wameshuhudia makabiliano makali na kurushiana risasi

image
na Radio Jambo

Habari13 May 2024 - 04:11

Muhtasari


•Watoto wawili waliuawa na wengine kujeruhiwa baada ya bomu kuanguka karibu na hospitali ya watoto katika mji wa magharibi wa Sudan wa El Fasher.

•Tangu Ijumaa, wakaazi wameshuhudia makabiliano makali na kurushiana risasi.

Watoto wawili waliuawa na wengine kujeruhiwa baada ya bomu kuanguka karibu na hospitali ya watoto katika mji wa magharibi wa Sudan wa El Fasher, shirika la Madaktari wasio na Mipaka-MSF limesema.

Mapigano yamezidi hivi majuzi katika vita vya kuudhibiti mji huo.

Ni kituo kikuu cha mwisho cha mijini katika eneo la Darfur ambacho kimesalia mikononi mwa jeshi.

Imekuwa ikipigana na Wanajeshi wa Rapid Support Forces (RSF) kwa zaidi ya mwaka mmoja, katika vita vya wenyewe kwa wenyewe ambavyo vimesababisha vifo vya maelfu ya watu na kuwalazimisha mamilioni kutoka kwa makazi yao.

Jeshi limeweza kushikilia El Fasher lakini hali ya wasiwasi imekuwa ikiongezeka huku RSF ikiuzingira mji huo tangu katikati ya mwezi uliopita na kutishia kushambuliwa.

Tangu Ijumaa, wakaazi wameshuhudia makabiliano makali na kurushiana risasi, mwandishi wa habari wa kujitegemea katika jiji hilo aliambia BBC.

Wakati fulani usiku wa kuamkia Jumapili mlipuko mbele ya Hospitali ya Watoto ya Babiker Nahar inayoungwa mkono na MSF huko El Fasher "ulisababisha kuporomoka kwa paa la chumba cha wagonjwa mahututi na vifo vya watoto wawili wanaopokea matibabu hapo, pamoja na baadhi ya walezi", shirika la MFS lilisema katika taarifa fupi iliyotumwa kwa BBC.

Wagonjwa pia walijeruhiwa na wale ambao wangeweza kutafuta usalama walifanya hivyo katika hospitali nyingine, ambayo tayari ilikuwa imechukua watu 160 waliojeruhiwa siku ya Ijumaa.

Haijabainika ni nani aliyehusika na shambulio hilo.

Sehemu ya kusini ya jiji, ambayo hapo awali ilichukuliwa kuwa salama na kimbilio la watu waliohamishwa, imekuwa ikichomwa moto.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved