logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gachagua hakufadhili kongamano la Limuru III- Kioni aweka wazi

Baadhi ya viongozi kutoka eneo hilo walidai kuwa "mtu fulani" alikuwa akifadhili hafla hiyo.

image
na

Habari30 May 2024 - 11:52

Muhtasari


  • Akizungumza Jumatano, Kioni alisema kongamano hilo lilitokana na juhudi za pamoja na uungwaji mkono wa wananchi kutoka eneo la Mlima Kenya.

Katibu mkuu wa Jubilee Jeremiah Kioni amekanusha ripoti kuwa kongamano la Limuru III lilifadhiliwa na Naibu Rais Rigathi Gachagua.

Akizungumza Jumatano, Kioni alisema kongamano hilo lilitokana na juhudi za pamoja na uungwaji mkono wa wananchi kutoka eneo la Mlima Kenya.

Alisisitiza kuwa hii ni mara ya kwanza kwa tukio hilo kuendeshwa na wananchi.

Kioni alisema kuwa watu hao walikuwa na maswala ambayo walitaka kushughulikia na ndivyo ilifanyika.

"Yeye (Gachagua) hakufanya hivyo. Haikufadhiliwa na mtu yeyote. Ilikuwa Limuru III iliyojifadhili yenyewe, tofauti na siku za nyuma.

“Watu walitumia rasilimali zao na walikuja kwa wingi na kutaka kuongea na walisema masuala yao,” alisema kwenye KTN News.

Baadhi ya viongozi kutoka eneo hilo walidai kuwa "mtu fulani" alikuwa akifadhili hafla hiyo.

Mkutano wa Limuru III ulifanyika Mei 17, 2024. Ulizaa muungano mpya wa Mlima Kenya uliopewa jina la Haki Coalition.

Muungano huo unaundwa na zaidi ya vyama 26 vya kisiasa kutoka eneo la Mlima Kenya.

Waandalizi wa mkutano wa Limuru III wa kijamii na kiuchumi na kisiasa walikuwa wamesema kuwa Gachagua na rais wa zamani Uhuru Kenyatta wanakaribishwa kuhudhuria kongamano hilo.

Kabla ya kongamano hilo, Gachagua alikuwa ametoa wito kwa Kioni na Karua kushauriana naye kuhusu masuala yanayohusiana na Mlima Kenya.

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved