logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Joto laua zaidi ya watu 50 nchini India kwa siku tatu

Takriban watu 33 walikufa katika jimbo la kaskazini la Uttar Pradesh mwishoni mwa juma kutokana na joto.

image
na SAMUEL MAINA

Habari03 June 2024 - 09:39

Muhtasari


  • •Takriban watu 33 walikufa katika jimbo la kaskazini la Uttar Pradesh mwishoni mwa juma kutokana na joto.

Zaidi ya watu 50 wamefariki dunia nchini India katika muda wa siku tatu zilizopita huku hali ya joto kali ikiendelea kukumba sehemu za nchi hiyo.

Takriban watu 33 walikufa katika jimbo la kaskazini la Uttar Pradesh mwishoni mwa juma kutokana na joto.

Katika jimbo la Odisha (Orissa), takriban watu 20 walikufa kutokanana wimbi kali la joto, afisa aliliambia shirika la habari la ANI.

Vingi vya vifo hivi viliripotiwa tarehe 1 Juni wakati India ilipopiga kura katika awamu ya mwisho ya upigaji kura kwa uchaguzi wake mkuu.

Matokeo ya uchaguzi huo yamepangwa kutangazwa tarehe 4 Juni.

Kila baada ya miaka mitano, India hufanya uchaguzi wake mkuu katika miezi ya kiangazi ya Aprili na Mei.

Lakini mwaka huu, hali ya joto imekuwa ikivunja rekodi, huku nchi ikikumbwa na mawimbi ya joto ya mara kwa mara, makali zaidi na marefu zaidi.

Wizara ya afya ya serikali kuu inasema kwamba kumekuwa na vifo 56 vilivyothibitishwa vya mawimbi ya joto kutoka 1 Machi hadi 30 Mei. Karibu visa 24,849 mawimbi ya joto viliripotiwa katika kipindi hicho.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved