logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wanandoa wavua kisanduku chenye shilingi milioni 13 katika ziwa

Walipofungua ndani ya sanduku hilo walikuta limejaa noti za $100 zilizoharibiwa na maji.

image
na Radio Jambo

Habari03 June 2024 - 06:30

Muhtasari


•James Kane na Barbie Agostini walirusha kamba ya kuvua yenye sumaku kwenye ziwa eneo la Queens siku ya Ijumaa na kuvuta kijisanduku.

•"Tulilitoa nje na ilikuwa ni rundo kubwa la mamia," aliongeza. "Hili ni rundo nene - zimelowa, zimeharibiwa sana," walisema.

Wanandoa "wanaovua kwa sumaku" wanasema wamevuta kijisanduku kilichokuwa na wastani wa $100,000 (£78,000) (Sh13milioni) kutoka ziwa la New York.

James Kane na Barbie Agostini walirusha kamba ya kuvua yenye sumaku kwenye ziwa eneo la Queens siku ya Ijumaa na kuvuta kijisanduku.

Walipofungua ndani ya sanduku hilo walikuta limejaa noti za $100 zilizoharibiwa na maji.

Walisema polisi imewaambia kuwa kisanduku hicho hakikuhusishwa na uhalifu wowote na kwamba wanaruhusiwa kuweka pesa hizo. BBC imeenda katika Idara ya Polisi ya New York (NYPD) ili itoe maoni.

"Tumepata visanduku vingi hapo awali," Bw Kane alisema. "Na kisha nikaona idadi ya noti na kufikiria: 'Hii haiwezekani.'

"Tulilitoa nje na ilikuwa ni rundo kubwa la mamia," aliongeza. "Hili ni rundo nene - zimelowa, zimeharibiwa sana."

"Hakukuwa na vitambulisho katika kijisanduku, wala namna ya kumpata mmiliki halisi,," Bi Agostini alisema. "[Polisi] walisema: 'Hongereni!'"

Uvuvi wa sumaku unahusisha kuvuta kamba yenye sumaku kali kupitia maziwa na mito na kuona kile kinachovutwa juu.

Wanandoa hao walisema walianza uvuvi wa sumaku wakati wa janga la Covid-19 na kuongeza kuwa siku za nyuma, wamewahi kupata maguruneti ya zama za Vita vya Pili vya Dunia, bunduki za karne ya kumi na tisa na pikipiki ya kubwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved