logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mbunge wa Mathira ajibu madai ya DP Gachagua, amtaka aseme ukweli kuhusu ugomvi wao

"Ni kweli, kuna mzozo kati ya Naibu Rais na mimi. Mzozo huo hauhusu baa zilizofungwa

image

Habari08 July 2024 - 12:02

Muhtasari


  • Wamumbi ambaye aliingia kwenye mitandao ya kijamii alipuuzilia mbali madai kwamba mzozo huo ulitokana na vita dhidi ya pombe haramu na kufungwa kwa baa kadhaa.

Mbunge wa Mathira Eric Wamumbi Jumapili alithibitisha kuwa kulikuwa na mtafaruku kati yake na Naibu Rais Rigathi Gachagua.

Wamumbi ambaye aliingia kwenye mitandao ya kijamii alipuuzilia mbali madai kwamba mzozo huo ulitokana na vita dhidi ya pombe haramu na kufungwa kwa baa kadhaa.

"Ni kweli, kuna mzozo kati ya Naibu Rais na mimi. Mzozo huo hauhusu baa zilizofungwa katika mji wa Karatina ambazo zimeacha mji huo kufa kwa miezi minne," alisema.

Alimsuta  DP kwa kutoa madai ya uwongo na kumsihi awaambie Wakenya ukweli kuhusu sababu halisi walizokuwa wakizozana.

Mwanasiasa huyo alisisitiza kuwa atasema ukweli na kuwaruhusu watu wa Mathira kuamua ni hadithi gani ni kweli. Hata hivyo hakufichua ni lini angeshiriki upande wake wa hadithi.

"Ni juu ya jambo kubwa zaidi ya hilo, anapaswa kusema ukweli na hakuna chochote isipokuwa ukweli," aliongeza.

Matamshi ya Wamumbi yalijiri saa chache baada ya Gachagua kumwita na kuapa kuchukua hatua kwa madai ya hujuma ya mradi wake kusitisha uuzaji wa pombe haramu katika eneo hilo.

Gachagua alizungumza wakati wa ibada katika eneo bunge hilo na kuongeza kuwa amewaagiza maafisa wote wa usalama kupuuza maagizo ya mbunge kuhusu kufungua tena baa.

"Mbunge hawezi kuwaelekeza maafisa wa usalama, ikiwa maafisa wa usalama kutoka eneo hili wanachukua maagizo kutoka kwa mbunge, tutawatia adabu," alisema.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved