logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mhubiri azuiliwa baada ya viungo vya mwili wa binadamu kupatikana garini mwake

Mhubiri azuiliwa kule Bungoma baada ya sehemu za mwili wa binadamu kupatikana kwa gari lake.

image
na Davis Ojiambo

Habari09 July 2024 - 06:55

Muhtasari


  • •Mhubiri mmoja anazuliwa na maafisa wa polisi baada ya sehemu za mwili wa binadamu kupatikana kwa gari lake.
  • •Wahudumu wa kuosha magari katika soko la Masikhu mjini Bungoma waligundua sehemu hizo za mwili kabla ya polisi kuitwa.

Polisi katika kaunti ya  Bungoma wanamshikilia mtu mmoja anayefahamika kuwa  mhubiri ambaye alipatikana na sehemu za mwili wa binadamu kwenye gari lake.

Maafisa kutoka Webuye mashariki walisema kuwa sehemu za mwili zilipatikana zikiwa zimefichwa kwenye katoni na wahudumu wa kuosha magari katika soko la Masikhu mjini Bungoma.

Mshukiwa aliyetambulika kwa jina la Levis Simiyu, anasemekana kuwa mchungaji katika kanisa la mtaa wa Ndivisi. Mhudumu alikuwa akiosha gari kabla ya  kuona  mguu wa binadamu uliotokezea nje,ukiwa umeungua kwa kiasi.

"Kijana huyo aliacha kazi yake tayari kustaafu mapema, hadi meneja wa kituo cha mafuta alipotazama sanduku la kutisha," polisi walisema.

Idara ya upelelezi wa makosa ya jinai (DCI) iliongeza kuwa polisi waliitwa baadaye kwenye eneo la tukio.

“Meneja alitoa taarifa mara moja kwa polisi katika kituo cha Webuye, ambao walifika kwa wakati kabla ya mwenye gari kuondoka."

Viungo vya miili hiyo vimepelekwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali ya Webuye kwa uchunguzi zaidi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved