logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Spika Kingi awaonya maseneta dhidi ya kutumia fursa ya kuuliza maswali kutengeneza video za tiktok

Maseneta wanajadili hoja ya kumtimua naibu wa rais Rigathi Gachagua mamlakani

image
na Brandon Asiema

Habari17 October 2024 - 15:05

Muhtasari


  • “Wakati umepewa nafasi ya kutaka ufafanuzi ama kuuliza swali, si wakati wa kupata video ya kuchapisha kwenye mtandao wa tik tok.”  Alisema Kingi.
  • Hatma ya kubanduliwa kwa Gachagua ipo mikononi mwa maseneta wanaotarajiwa kutoa uamuzi Alhamisi 17, ikiwa atabanduliwa 

Spika wa bunge la seneti Amason Kingi amewasihi maseneta kutumia  fursa wanayopewa kuuliza maswali vyema na wala si kutumia nafasi hiyo kufanya utani ili video zisambae kwenye mtandao wa tik tok.

Kingi amesema hayo wakati wa kikao ambapo maseneta wanajadili hoja ya kumtimua naibu wa rais Rigathi Gachagua kutoka mamlakani, hoja iliyowasilishwa bungeni humo baada ya bunge la kitaifa kuidhinisha kubanduliwa kwake.

“Wakati umepewa nafasi ya kutaka ufafanuzi ama kuuliza swali, si wakati wa kupata video ya kuchapisha kwenye mtandao wa tik tok.”  Alisema spika Kingi.

Mwenyekiti huyo anayeongoza kusikilizwa kwa madai yaliyowasilishwa na mbunge wa Kibwezi Magharibi Mwengi Mutuse,  amewarai maseneta kutoaibisha bunge la seneti katika vikao hivyo muhimu vilivyoanza Jumatano 16.

Maseneta wamefanya kikao kwa siku ya pili wakijadili kuhenguliwa kwa naibu wa rais ambapo wamekuwa wakihakiki maswala yaliyoibuliwa na mwasilishaji wa hoja hiyo na mawakili wa naibu wa rais.

Hatma ya kubanduliwa kwa Gachagua ipo mikononi mwa maseneta wanaotarajiwa kutoa uamuzi Alhamisi 17, ikiwa atabanduliwa.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved