logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mshtuko huku Nuru Okanga akivua nguo hadharani kusherehekea kutimuliwa kwa Rigathi Gachagua

Okanga alishindwa kuficha furaha yake siku ya Ijumaa jioni wakati akisherehekea kuondolewa madarakani kwa naibu rais Rigathi Gachagua.

image
na Samuel Mainajournalist

Habari19 October 2024 - 12:28

Muhtasari


  • Okanga ambaye ni mwanachama maarufu wa kikao cha Bunge la Mwananchi alisimulia furaha yake kwa wanachama wenzake na watazamaji huku akibainisha kuwa Gachagua hakufaa kushikilia kiti hicho.
  • “Wacha nitoe nguo Gachagua, Gachagua, Gachagua!!” Nuru Okanga alifoka kabla ya kuvua suruali yake.

Mfuasi maarufu wa ODM na kinara wa chama hicho Raila Odinga, Nuru Okanga alishindwa kuficha furaha yake siku ya Ijumaa jioni wakati akisherehekea kuondolewa madarakani kwa naibu rais Rigathi Gachagua.

Okanga ambaye ni mwanachama maarufu wa kikao maarufu cha Bunge la Mwananchi kinachofanyika katika Kiwanja cha Jacaranda, jijini Nairobi alisimulia furaha yake kwa wanachama wenzake na watazamaji huku akibainisha kuwa Gachagua hakufaa kushikilia kiti hicho.

Alibainisha kuwa alifurahishwa sana na hatua ya bunge na seneti kumtimua Gachagua, kiasi kwamba alikuwa tayari kuvua nguo zake ili kudhihirisha hilo.

“Wacha nitoe nguo Gachagua, Gachagua, Gachagua!!” Nuru Okanga alifoka kabla ya kuvua suruali yake.

“Gachagua ameenda nyumbani*2, Mimi nilisema lazima Wakenya wajue Gachagua ameenda nyumbani,” aliendelea kusema huku suruali yake ikiwa chini kwenye miguu yake.

Mfuasi huyo sugu wa chama cha ODM aliendelea kueleza kuwa hakufurahishwa na mtazamo wa Gachagua kuhusu jinsi nchi inavyofaa kuongozwa.

“Mimi niko na furaha kwa sababu tumempeleka Mathira mtu ambaye amesema Kenya ni kampuni. Kumbe Bondo ni karibu kuliko Mathira, Gachagua*3 mambo yake imeisha,” alisema.

Haya yalijiri kufuatia kuondolewa madarakani kwa naibu rais Rigathi Gachagua na seneti, na kuteuliwa kwa naibu rais mpya Kindiki Kithure na rais William Ruto.

Maseneta wengi mnamo  Alhamisi usiku waliunga mkono kuondolewa kwa Naibu Rais Rigathi Gachagua licha ya upande wa utetezi kuonekana kufanya vizuri katika kazi yao..

Maseneta waliidhinisha mashtaka matano kati ya 11 yaliyotolewa dhidi ya Gachagua.

"Seneti imeazimia kumuondoa afisini kwa kumwondoa madarakani MHE. Rigathi Gachagua, Naibu Rais wa Jamhuri ya Kenya. Kwa hiyo, H.E. Rigathi Gachagua akoma kushikilia wadhifa huo,” Spika Amason Kingi alisema.

Mashtaka yaliyoidhinishwa ni pamoja na; shtaka la maoni ya Wanahisa, mashtaka manne ya kuingilia Uhuru wa Majaji na mashtaka matano ya Sheria ya Uwiano na Uadilifu wa Kitaifa.

Pia walishikilia misingi ya sita na tisa kuhusu uhalifu chini ya Sheria ya Uwiano wa Kitaifa na Utovu wa Maadili Mkubwa.




RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved