Jengo
la orofa nyingi lenye nyumba za makazi na biashara kadhaa limeripotiwa kuporomoka
katika eneo la Kahawa West, Nairobi siku
ya Jumapili adhuhuri.
Familia
kadhaa zinahofiwa kukwama ndani ya jengo hilo ambalo kuanguka kwake
kulirekodiwa katika video zinazovuma kwenye mitandao ya kijamii.
Shirika
la Msalaba Mwekundu la Kenya limesema kuwa timu imetumwa kusaidia shughuli ya
uokoaji.
"Timu
ya mashirika mengi ya kukabiliana na matukio kwa sasa inajibu kufuatia
kuporomoka kwa jengo katika eneo la Kahawa Magharibi, Kaunti ya Nairobi, ambapo
watu wanahofiwa kunaswa." Msalaba Mwekundu alisema katika taarifa.
Taarifa
zaidi zitafuata punde tutakapozipata...