logo

NOW ON AIR

Listen in Live

RIP! Jaji Mkuu Martha Koome atangaza kifo cha Hakimu Mkuu Bernard Kipyegon

Marehemu alikuwa hakimu mkuu katika Mahakama ya Sheria ya Molo hadi wakati wa kifo chake.

image
na Samuel Mainajournalist

Habari22 October 2024 - 11:19

Muhtasari


  • Habari za kifo cha Rugut zilithibitishwa na Jaji Mkuu Martha Koome Jumanne asubuhi ambapo alimuomboleza kwa niaba ya Idara ya Mahakama.
  • Rugut alianza taaluma yake na mahakama mnamo Julai 13, 2012 alipoteuliwa kuwa hakimu mkazi na kutumwa katika Mahakama za Sheria za Bondo.

Idara ya mahakama ya Kenya kwa mara nyingine imetumbukia katika hali ya majonzi kufuatia kifo cha hakimu Mh. Bernard Kipyegon Rugut.

Habari za kifo cha Rugut zilithibitishwa na Jaji Mkuu Martha Koome Jumanne asubuhi ambapo alimuomboleza kwa niaba ya Idara ya Mahakama.

Marehemu alikuwa hakimu mkuu katika Mahakama ya Sheria ya Molo hadi wakati wa kifo chake.

“Kwa masikitiko makubwa na moyo mzito natangaza kifo cha Mhe. Bernard Kipyegon Rugut, Hakimu Mkuu katika Mahakama za Sheria za Molo,” Koome alitangaza katika taarifa yake.

“Kwa niaba ya Mahakama, napenda kumpa pole mke wake, Mhe. Purity Koskey Rugut wa Mahakama ya Sheria ya Kabarnet, watoto wao, familia nzima, jamaa, marafiki, na wafanyakazi wenzake wa Mhe. Rugut wakati huu mgumu sana, "aliongeza.

Kulingana na Jaji Mkuu, Rugut alianza taaluma yake na mahakama mnamo Julai 13, 2012 alipoteuliwa kuwa hakimu mkazi na kutumwa katika Mahakama za Sheria za Bondo.

"Kwa miaka mingi, alihudumu kwa kujitolea thabiti katika vituo mbalimbali, ikiwa ni pamoja na Mahakama ya Sheria ya Ndiwa na Kericho, akionyesha kujitolea kwa dhati kwa kanuni za haki. Hivi majuzi, tangu Mei 2, 2023, alihudumu kama Hakimu Mkuu katika Mahakama za Sheria za Molo,” Koome alisema.

Jaji mkuu aliendelea kumtambua marehemu Rugut kwa bidii yake, haki na weledi wake katika majukumu yake yote ya mahakama.

"Kuaga kwake sio tu hasara kubwa kwa familia yake lakini pia kwa Mahakama na jamii alizotumikia kwa uaminifu. Mawazo na sala zetu ziko pamoja na wapendwa wake tunapoomboleza kifo cha afisa wa mahakama aliyejitolea ambaye urithi wake wa utumishi unaendelea kututia moyo sisi sote. Roho yake ipumzike kwa amani ya milele,” Koome alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved