logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kanisa la Kiangilikani launga mkono maaskofu wa kanisa Katoliki katika kuwajibisha serikali

Hii inajiri baada ya kanisa Katoliki kufokewa na baadhi ya viongozi wanaoegemea upande wa serikali

image
na Brandon Asiema

Habari18 November 2024 - 13:13

Muhtasari


  • Sapit amejitenga na habari katika vyombo vya habari kuwa kanisa la ACK halikubaliani na maaskofu wa kanisa Katoliki katika kuwajibisha serikali.
  • Katika taarifa yake kwa vyumba vya habari, Sapit alisema tabaka la kisiasa na wale walio serikalini wanahitaji kushuka kwa kile alichokiita ‘kutoka kwa farasi wao wa juu’,  na badala yake kusikiliza kwa mara moja, badala ya kuonekana kuendeleza utamaduni wa kawaida wa kutokujali.

caption

Kanisa la Kiangilikani la Kenya limesema kuwa linaunga mkono uwajibishaji kwa serikali kutoka kwa kanisa la Katoliki lililofanywa na baraza la maaskofu wa Kikatoliki wiki jana.

Katika taarifa yake kwa vyumba vya habari, Sapit alisema tabaka la kisiasa na wale walio serikalini wanahitaji kushuka kwa kile alichokiita ‘kutoka kwa farasi wao wa juu’,  na badala yake kusikiliza kwa mara moja, badala ya kuonekana kuendeleza utamaduni wa kawaida wa kutokujali.

"Watawala hawahitaji mihadhara lakini huduma na ushiriki wa uaminifu. Tafadhali jikite katika kutoa uongozi kwa njia ya maana na kwanza ushughulikie maelfu ya matatizo ambayo yanaidhalilisha nchi,”  Ole Sapit alisema.

Katika taarifa yake Sapit alidokeza kuwa mtindo mpya wa ufadhili wa chuo kikuu haujafanya kazi tangu kuasisiwa miezi kadhaa iliyopita.

"Vyuo vikuu vya umma vinafanya kazi kwa shida. Ucheleweshaji wa mara kwa mara wa kutoa ufadhili kwa wanafunzi umeendelea kudhoofisha uendeshaji bora wa shule za umma.”

Vile vile Askofu huyo mkuu, amelalamikia mageuzi yaliyofanywa kutoka kwa mfumo wa bima ya afya ya NHIF kuingia mamlaka ya afya ya jamii SHA, akisema kuwa Wakenya wanazidi kuteseka na mabadiliko hayo kwa kuwa mabadiliko hayo bado hayajakuwa laini.

Ole Sapit  pia ameitaka serikali kuwajibikia visa vya kupotea kwa Wakenya kupitia kutekwa nyara bila sababu pamoja na mauaji ambayo hayajatatuliwa.

Sapit aliongeza kuwa Wakenya wanatatizika kulipa kodi, matatizo ya ukosefu wa ajira na mazingira duni ya biashara.

Ujumbe wa Ole Sapit unajiri baada ya viongozi wanaoegemea upande wa serikali kukashifu uwajibishaji wa werikali wa wazi kutoka kwa  viongozi wa kidini nchini.

Aidha Sapit amejitenga na habari katika vyombo vya habari kuwa kanisa la ACK halikubaliani na maaskofu wa kanisa Katoliki katika kuwajibisha serikali

Alisema maaskofu wamezungumza mawazo ya Wakenya na kueleza ukweli kwa uaminifu wa mambo yalivyo mashinani.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved