logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gari moja kwenye msafara wa maiti yafanya ajali na kuuwa mtu 1 na kujeruhi wengine 2

Waombolezaji walikuwa wakisindikiza maiti ya mhanga wa kuporomoka kwa ghorofa jijini Dar es Salaam

image
na Brandon Asiema

Habari22 November 2024 - 08:28

Muhtasari


  • Dereva wa gari hilo alipoteza mweleko alipokuwa analipita gari lingine na kugonga kikingi  ivyo kusababisha ajali hiyo.
  • Watu zaidi ya 10 walipoteza maisha yao kupitia ajaliya kuporomoka kwa ghorofa wiki iliyopita.

caption

Mtu mmoja ameangamia katika ajali ya barabarani nchini Tanzania baada ya gari alimokuwa akisafiria kupoteza mwelekeo na kubingiria mara kadhaa barabarani.

Gari hilo lilikuwa sehemu ya msafara wa magari yaliyokuwa yamewabeba waombelezaji waliokuwa wakipeleka maiti ya jamaa mmoja aliyekufa katika mkasa wa jingo la kibiashara kuporomoka mtaani Kariakoo kwenye jiji la Dar es Salaam.

Akidhibitisha kisa cha ajali hiyo, kamishna msaidizi wa polisi wa mkoa wa Mbeya Benjamin Kuzaga alisema kuwa watu wengine wawili akiwemo dereva walipata majeraha na sasa wanaendelea kupokea matibabu.

Kamishna msaidizi huyo wa polisi alisema kwamba ajali hiyo ilitokea wakati dereva wa gari lililofanya ajali alishindwa kulidhibiti wakati alikuwa analipita gari linguine. Taarifa ya polisi ilisema kwamba baada ya dereva kushindwa kudhibiti gari, aligonga kikingi  na kupinduka hivyo kusababisha kifo cha mtu mmoja na majeruhi wawili akiwemo.

Gari lililofanya ajali lilikuwa sehemu ya magari matatu yaliyokuwa katika msafara wa kupeleka maiti  katika mji wa Tunduma kwa ajili ya mazishi ya mhanga wa wa ghorofa iliyoporomoka Kariakoo.

Zaidi ya watu 13 walipoteza maisha katika mkasa wa kuporomoka kwa ghorofa jijini Dar es Salaam wiki jana.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved