logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Afisa wa polisi anatafutwa kwa kumfyatulia jamaa mmoja risasi katika sehemu ya burudani

Afisa huyo anadaiwa kuwa mkuu wa kituo kimoja cha polisi katika kaunti ya Trans Nzoia

image
na Brandon Asiema

Habari27 November 2024 - 14:18

Muhtasari


  • Polisi walipata ganda ya risasi inayodaiwa kutumika na mshukiwa ambayo itawawasidia katika uchunguzi.
  • Kiini kilichosababisha ufyatuaji wa risasi hakijabainika bado wakati mwathiriwa anapata nafuu katika hospitali ya misheni ya Letien.

caption

Maafisa wa upelelezi kutoka kaunti ndogo ya Sotik wanamtafuta afisa mmoja wa polisi anayesemekana kuwa OCS katika kituo kimoja cha polisi katika Kaunti ya Trans Zoia kwa kumpiga risasi mkaazi wa eneo la Sotik kwa jina Charles Mutai tumboni mwendo wa saa saba usiku wa Jumanne katika kisa kilichotokea katika sehemu moja ya burudani iliyoko Kapcherany.

Kisa hicho kinadaiwa kutokea wakati  afisa huyo alikuwa katika likizo fupi nyumbani ila kiini cha kumpelekea kumfyatulia mwathiriwarisasi hakijajulikana.

Kufuatia kupigwa risasi, Mutai alikimbizwa katika hospitali ya Kapkatet kwa huduma ya kwanza kabla ya kuhamishiwa katika Hospitali ya Misheni ya Litein kwa matibabu zaidi. Kwa mujibu wa polisi, mwathiriwa anaendelea kupokea matibabu na sasa amepata nafuu angalau.

Maafisa wa upelelezi waliotembelea eneo la uhalifu walipata mabaki ya risasi ya milimita 9 iliyotumika ambayo itakuwa muhimu katika uchunguzi wao.

Maafisa wanaoendesha uchunguzi huo wamemtaka mshukiwa kujisalimisha mwenyewe ili kuhojiwa kubaini sababu iliyopelekea kumpiga mwathiriwa risasi.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved