Shirika la ndege la Jambojet limethibitisha tukio ambapo ndege ya shirika hilo iligonga nguzo wakati ikitengenezwa usiku katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta siku ya Jumatatu.
Kulingana na Jambojet, ndege hiyo iliteleza kwenye njia ilipokuwa imeegeshwa, ikigonga nguzo kabla ya kusimama.
"Timu yetu inafanya kazi kwa bidii na mamlaka kuchunguza suala hilo na kuhakikisha hatua zote muhimu zinachukuliwa kuzuia kutokea tena," walibainisha katika taarifa.
Pia walisema hakuna wafanyikazi waliojeruhiwa, na ndege hiyo imeondolewa kutoka kwa huduma hadi itakapoondolewa.
Shirika hilo la ndege pia lilisema kuwa tukio hilo lilisababisha kuchelewa kwa baadhi ya safarikya matatizo ya ndege na kwamba abiria wote walioathirika watajulishwa.
Jambojet imewahakikishia abiria usalama wao na kueleza kuwa wanahakikisha shughuli zote za uchunguki zunafanyika kwa viwango vya juu.