logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jambojet yakatiza safari zake huku ndege ikigonga nguzo JKIA

Kulingana na Jambojet, ndege hiyo iliteleza kwenye njia ilipokuwa imeegeshwa, ikigonga nguzo kabla ya kusimama.

image
na Davis Ojiambo

Habari03 December 2024 - 12:24

Muhtasari


  • Shirika hilo la ndege pia lilisema kuwa tukio hilo lilisababisha kuchelewa kwa baadhi ya safarikya matatizo ya ndege na kwamba abiria wote walioathirika watajulishwa.


Shirika la ndege la Jambojet limethibitisha tukio ambapo ndege ya shirika hilo iligonga nguzo wakati ikitengenezwa usiku katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta siku ya Jumatatu.

Kulingana na Jambojet, ndege hiyo iliteleza kwenye njia ilipokuwa imeegeshwa, ikigonga nguzo kabla ya kusimama.

"Timu yetu inafanya kazi kwa bidii na mamlaka kuchunguza suala hilo na kuhakikisha hatua zote muhimu zinachukuliwa kuzuia kutokea tena," walibainisha katika taarifa.

Pia walisema hakuna wafanyikazi waliojeruhiwa, na ndege hiyo imeondolewa kutoka kwa huduma hadi itakapoondolewa.

Shirika hilo la ndege pia lilisema kuwa tukio hilo lilisababisha kuchelewa kwa baadhi ya safarikya matatizo ya ndege na kwamba abiria wote walioathirika watajulishwa.

Jambojet imewahakikishia abiria usalama wao na kueleza kuwa wanahakikisha shughuli zote za uchunguki zunafanyika kwa viwango vya juu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved