logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Watu 12 wameaga na 3,970 kukosa makao kutokana na mvua inayonyesha nchini

Katika Kaunti ya Kisumu, Katibu huyo wa kudumu pia alitembelea Kambi ya Watu Waliohama makwao ya Ogenya, inayo na familia 1,973.

image
na Davis Ojiambo

Habari04 December 2024 - 16:30

Muhtasari


  • Mvua ambayo imekuwa ikinyesha katika maeneo mbali mbali ya nchi imesababa vifo vya zaidi ya watu 12 na kuacha zaidi ya familia 3,970 bila makao.

BIGAMBO: Swift emergency response to Nairobi flooding, leaders ...


Mvua ambayo imekuwa ikinyesha katika maeneo mbali mbali ya nchi imesababa vifo vya zaidi ya watu 12 na kuacha zaidi ya familia 3,970 bila makao.

Katibu wa kudumu wa Usalama wa Ndani na Utawala wa Kitaifa, Dkt. Raymond Omollo amekuwa katika ziara ya kukagua athari za mafuriko. Siku ya Jumanne alikagua maeneo yaliyoathiriwa na mafuriko katika kaunti za Busia na Kisumu ili kutathmini kiwango cha uharibifu, kusimamia usambazaji wa misaada, na kuwasiliana na familia zilizoathirika.

Katika Kaunti Ndogo ya Bunyala, Dkt. Omollo alitembelea Shule ya Msingi ya Lunyofu, ambayo kwa sasa inahifadhi familia 500 zilizohamishwa. Alisimamia usambazaji wa chakula na bidhaa zisizo za chakula, ikiwa ni pamoja na mchele, maharagwe, blanketi, na vifaa vya matibabu, akisisitiza dhamira ya serikali kwa usalama na kuokoa familia zilizoathirika. Akikiri kwamba zaidi ya familia 3,000 huko Busia zimeathiriwa na mafuriko, PS Omollo alisisitiza haja ya makazi endelevu katika maeneo salama.

Pia alitangaza mipango ya uendelezaji wa miundombinu, ikiwa ni pamoja na upanuzi wa lamba (dykes) na ujenzi wa bwawa la juu ya mto ambalo ni Kilomita 4-5 ili kudhibiti mtiririko wa maji na kusaidia unyunyiziaji mashamba maji na matumizi ya nyumbani.

PHOTOS] Hop, skip and jump as heavy rains leave city roads impassable


“Wakati mvua zinatarajiwa kupungua hivi karibuni, lazima tuwe macho na kuzingatia maagizo ya usalama ya serikali. Hii ni pamoja na kuepuka maeneo hatari ikiwa ni pamoja na mabwawa, barabara na madaraja yanayochukuliwa kuwa si salama na kufuata notisi za kuhama,” alisema Dkt Omollo.

Katika Kaunti ya Kisumu, Katibu huyo wa kudumu pia alitembelea Kambi ya Watu Waliohama makwao ya Ogenya, inayo na familia 1,973. Omollo aliwataka wakazi wa Ogenya kushiriki katika Siku ya Chifu ya Utekelezaji wa Hali ya Hewa, inayofanyika kila Ijumaa ya kwanza ya mwezi, na kukumbatia mipango ya upandaji miti.

"Upanzi wa miti ni muhimu kwa kulinda mazingira yetu, kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi, na kutatua changamoto za usalama wa chakula," alisema, akitoa wito wa umoja katika kukumbatia miradi ya maendeleo.

Omollo alipongeza mashirika mbalimbali ya kukabiliana na majanga, ikiwa ni pamoja na Kituo cha Kitaifa cha kushughulikia Mikasa na Msalaba Mwekundu, kwa hatua zao za haraka na zinazofaa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved