logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jamaa aliyekiri kuwa hakuna Mungu ahofia maisha yake baada ya kumaliza kifungo jela

Mkosoaji huo wa kidini alijipata pabaya baada ya kundi la mawakili kuwasilisha ripoti kwa polisi kuhusu ujumbe aliokuwa amechapisha kwenye mtandao wa facebook.

image
na Brandon Asiema

Habari08 January 2025 - 15:54

Muhtasari


  • Bala alikufukuru kuwa Muislamu mwaka wa 2024.
  • Amehudumu jela miaka minne tangu kundi la mawakili kumshtaki kwa polisi na kufunguliwa mashtaka.


Mwanamume mwenye umri wa miaka 40 anahofia maisha yake siku chache baada ya kumaliza kuhudumia kifungo chake jela cha miaka minne kwa kukufuru.

Mubarak Bala alihukumiwa kifungo cha miaka minne jela baada ya kupatikana na hatia na mahakama moja nchini Nigeria. Bala alikiri makossa yote kumi na manne aliyoshtakiwa nayo kuhusu chapisho alilobandika kwenye ukuasa wake wa mtandao wa Facebook.

Jamaa huyo mkama Mungu ambaye ni maarufu Zaidi nchini Nigeria anahofia usalama wake baada ya kumaliza kifungu jela na kuachiliwa huru. Kwa mujibu wa shirika la habari la kimataifa la BBC, Mubarak Bala alisema kuwa wasiwasi kuhusu usalama wa maisha upo kila wakati.

Jamaa huyo ambaye awali alikuwa mshiriki wa dini ya Kiislamu, alikana uwepo wa Mungu mwaka wa 2014.

Akieleza kuhusu jinsi maisha yake yalikuwa wakati akihudumia kifungo gerezani, Bala alisema kuwa kuna wakati alikuwa anahofia maisha yake kutoka kwa wafungwa wengine akilini akiwaza ikiwa angeliwahi kumaliza kifungo chake na kutoka gerezani akiwa hai.

Hofu ya Bala kwa mujibu wake ilitokana na kuwa jela ya mwanzoni alikokuwa anazuiliwa kaskazini mwa Nigeria ilikuwa na wafungwa wengi wa dini ya Kiislamu. Eneo hilo la mji wa Kano linatambulika kwa kuwa na wafuasi wengi la Kiislamu.

Mkosoaji huo wa kidini alijipata pabaya baada ya kundi la mawakili kuwasilisha ripoti kwa polisi kuhusu ujumbe aliokuwa amechapisha kwenye mtandao wa facebook.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved