logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kisii: Polisi Waanzisha Uchunguzi Kisa Cha Mama Kuchapwa Na Jirani Kwa Kuiba Unga

Mwanamke huyo anatuhumiwa kwa kuchukua unga wa shilingi 150 kutoka kwa nyumba ya mama mzee kabla ya kuanza kuchapwa bila kupewa nafasi ya kujieleza.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari15 January 2025 - 08:52

Muhtasari


  • Inaarifiwa kwamba jirani huyo alimshuku kwa kuiba unga ngano wa kilo mbili kabla ya kuanza kumchapa.
  • Mwanamke huyo anatuhumiwa kwa kuchukua unga wa shilingi 150 kutoka kwa nyumba ya mama mzee kabla ya kuanza kuchapwa bila kupewa nafasi ya kujieleza.



POLISI katika kaunti ya Kisii wameanzisha uchunguzi kufuatia kisa cha kutamausha ambacho kilinaswa kwenye video mwanamume mmoja alimchapa viboko mwanamke kwa kudaiwa kuiba unga wa ngano.


Kwa mujibu wa ripoti, kisa hicho kilitokea katika Eneobunge la Bomachoge Borabu ambapo mwanamke huyo alionekana akichaopwa viboko na mateke na jirani yake, huku akiwa amempakata mwanawe mdogo mikononi.


Inaarifiwa kwamba jirani huyo alimshuku kwa kuiba unga ngano wa kilo mbili kabla ya kuanza kumchapa.


William Kaibet, mkuu wa polisi Kenyenya alithibitisha kupokea ripoti hiyo na kusema kwamba uchunguzi umeanzisha kumsaka mwanamume aliyenaswa kwenye video hiyo akimshambulia mwanamke huyo.


“Hicho kitendo ni lazima mtu awajibishwe mbele ya sheria. Na nadhani tukipata taarifa zaidi tutawajulisha,” alisema.


Mwanamke huyo anatuhumiwa kwa kuchukua unga wa shilingi 150 kutoka kwa nyumba ya mama mzee kabla ya kuanza kuchapwa bila kupewa nafasi ya kujieleza.


Majirani wenzake walieleza kwamba anaishi na ulemavu katika hali ya uchochole, jambo linalowafanya watu kumdharau.


“Hawa watu walisimama hapa nje na huyu mzee alikuwa anamchapa akaniambia niingie kwa nyumba nimwambie atoke nje aelezee kwa nini alipatikana nyumba ya mama akiiba unga wa ngano. Hata nilihuzunika mimi sana kwa maana haya ni madharau kwa sababu waliona hajiwezi ndio wamfanyie vibaya,” jirani mmoja alieleza huku akitoa wito kwa njia ya kumsaidia huyo mwanamke kupatikana.


Ni kisa ambacho kimezua gadhabu miongoni mwa wananchi mitandaoni, huku wakitoa wito kwa mwanamume aliyenaswa kwenye video akimchapa kuchukuliwa hatua za haraka kisheria.


Kudhalilishwa kwa mwanamke huyo kunajiri wakati ambapo nchini Kenya kumeshuhudiwa jinamizi la unyanyasaji wa kijinsia na mauaji dhidi ya wanawake, jambo ambalo mashirika mbalimbali ya kutetea haki za binadamu yametoa wito kwa serikali kutafuta njia madhubuti kupata mwafaka wake na kukomesha mauaji ya wanawake mikononi mwa wanaume na watu wa karibu.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved