logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Danstan Omari Atangaza Kuwania Useneta Nairobi 2027, Ataka Sifuna Kuwania Ugavana

"Huu ni wakati wa Sifuna kuwa gavana, na kwa hivyo, nitakuwa katika kinyang'anyiro cha kuchukua wadhifa wa Sifuna ili mwaka wa 2032, niwe pia gavana wa Nairobi."

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari22 January 2025 - 16:58

Muhtasari


  • Wakili huyo alisema Nairobi ni jiji kubwa barani Afrika na ndipo Rais anapoishi, na kuongeza kuwa linahitaji mtu thabiti, aliye makini na aliye na wasifu.
  • Alisema kuwa atakuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa pesa zinazotolewa jijini zinatumika ipasavyo kwa maendeleo ikiwa atanyakua kiti cha useneta.



WAKILI Danstan Omari ametangaza nia ya kuwania kiti cha useneta wa Nairobi 2027. Wakili huyo alisema kuwa Kaunti ya Nairobi inamhitaji akisema yeye ni mwaniaji thabiti wa nafasi hiyo.


Katika video iliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii alasiri ya Jumatano, Omari alisema, "Nairobi inahitaji mtu imara kuwa seneta; siasa za Nairobi ziko hivi; katika uchaguzi wa kwanza chini ya katiba mpya 2013, Evans Kidero alikuwa gavana na Mike Sonko alikuwa seneta 2017, Sonko alikua gavana huku Jonson Sakaja akiwa seneta 2022 Sakaja akawa gavana na Edwin Sifuna akawa seneta.”


"Huu ni wakati wa Sifuna kuwa gavana, na kwa hivyo, nitakuwa katika kinyang'anyiro cha kuchukua wadhifa wa Sifuna ili mwaka wa 2032, niwe pia gavana wa Nairobi."


Wakili huyo alisema Nairobi ni jiji kubwa barani Afrika na ndipo Rais anapoishi, na kuongeza kuwa linahitaji mtu thabiti, aliye makini na aliye na wasifu.


Alisema kuwa atakuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa pesa zinazotolewa jijini zinatumika ipasavyo kwa maendeleo ikiwa atanyakua kiti cha useneta.


"Nataka kuingia kama Danstan Omari, ambaye amekuwa kortini na kuwatetea wachuuzi, wapiga debe, waendesha bodaboda na jumuiya za wafanyabiashara wanaoanza kutoka biashara ndogo zaidi ya Sh5 hadi rasilimali za shilingi bilioni. Hiyo ndiyo sauti inayokosekana katika Seneti. ," aliongeza.


Wakili huyo aliongeza kuwa alianza kazi yake huko Nyamira, akahamia Nairobi, na sasa ni mtu wa kimataifa.


"Iwapo nitasimama kama mgombea binafsi au kwenye chama chochote, nitauza sera na nyadhifa zangu kama Danstan Omari," wakili huyo aliongeza.


Wakili wa jiji amewawakilisha wateja mbalimbali katika kesi kuanzia kusababisha fujo katika maandamano hadi mauaji.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved