logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Nairobi Ina’sink!”: Babu Asikitika Kuona Bodaboda Akiopoa Pikipiki Kutoka Majini

Owino alisema kwamba Sakaja ameshindwa kutatua suala la mabomba ya kupitisha maji chafu na kusababisha mafuriko kushuhudiwa

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari31 January 2025 - 07:40

Muhtasari


  • Owino alisema kwamba Sakaja ameshindwa kutatua suala la mabomba ya kupitisha maji chafu na kusababisha mafuriko kushuhudiwa 



MBUNGE wa Embakasi Mashariki Babu Owino ameonyesha sikitiko lake kwa wakaazi wa Nairobi na haswa watumizi wa barabara nyakati hizi za mvua nyingi.


Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Babu Owino alichapisha picha ya mwendesha bodaboda mmoja aliyepigwa picha akijaribu kuiokoa pikipiki yake kutoka dimbwi la maji barabarani.


Owino alisema kwamba ni sikitiko kubwa kwa mwendesha bodaboda huyo kwani sasa huenda pikipiki yake imeharibika injini kutokana na kuzama kwenye maji barabarani.


Mbunge huyo anayedaiwa kuwa mbioni kujitosa katika kinyang’anyiro cha ugavana Nairobi alionekana kuulaumu uongozi wa jiji akisema kwamba gavana Sakaja ameshindwa kazi.


Owino alisema kwamba Sakaja ameshindwa kutatua suala la mabomba ya kupitisha maji chafu na kusababisha mafuriko kushuhudiwa kwenye barabara nyingi za Nairobi pindi mvua zinaponyesha.


“Moyo wangu unauma ninapomuona huyu mwendesha Bodaboda anayetegemea mashine hii kujipatia riziki; kulipia karo ya shule kwa watoto wake, kununua chakula, kulipa karo ya kila mwezi na kulipia gharama nyinginezo.”


“Mtu huyu anapata takriban 200/- tu kwa siku baada ya kununua mafuta lakini pikipiki yake haitafanya kazi tena kwa sababu injini imezama ndani ya maji kutokana na mfumo mbovu wa mifereji ya maji jijini Nairobi ambayo inaletwa na Uongozi duni kutoka kwa Gavana asiye na uwezo.”


“Wengi wa waendesha Bodaboda huchukua pikipiki hizi kwa mkopo na lazima walipe bila kujali hatari yoyote ya kikazi inayowapata. Tuna jumla ya bajeti ya shilingi Bilioni 42 lakini Gavana hafanyi lolote, ni mzuri tu kwa visingizio. Wanairobi wasimchague tena asiye mwanataaluma katika Nafasi hii. #Nairobi inazama,” Owino alisema.


Katika kipindi cha wiki moja, Nairobi sawa tu na maeneo mengine nchini yamekuwa yakishuhudia mvua nyingi ambazo idara ya utabiri wa hali ya hewa imesema kwamba mvua hizo zitakata kuanzia wikendi hii.


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved