MBUNGE wa Embakasi Mashariki amefichua kwamba safari yake ya hivi majuzi katika taifa la Tanzania iliishia kwake kuzuiliwa kwa Zaidi ya saa tatu akituhumiwa kuwa ni mmoja wa watu wanaotafutwa na Interpol.
Owino alifichua haya hivi majuzi
wakati wa kikao chake cha mwanablogu Kogi kwenye chaneli yake.
Mbunge huyo alidai kwamba baada ya
kutua katika uwanja wa ndege jijini Dar es Salaam, alishtukia akizuiliwa na
kuonyeshwa kwamba jina lake lilikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wakitafutwa na
Interpol - shirika la kimataifa linalosaidia polisi kufanya kazi pamoja ili
kupambana na uhalifu.
“Nilikwenda Tanzania, unajua nini
kilitokea nilipofika Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam? Nilipowasilisha hati
yangu ya kusafiria kwa ajili ya kibali cha uhamiaji waliandika, “Interpol
Wanted List.” Sikuruhusiwa kuingia Tanzania, niliwekwa kizuizini huko kwa saa
tatu kwa sababu walidai nilikuwa kwenye Orodha ya Wanaotafutwa ya Interpol ya
Tanzania,
nikasema sijawahi iba hata kuku, shida hap ani gani?” Babu alifunguka.
Alifuatisha
klipu fupi kutoka kwa maongezi hayo kwenye kurasa zake mitandaoni akitoa wito
kwa rais wa taifa hilo, Samia Suluhu Hassan kumuomba msamaha mara moja kwa
kudhalilishwa kwake.
“Inashangaza
sana jinsi Tanzania iliweka jina langu kwa watu wanaotafutwa Zaidi na Interpol.
Rais Samia ana deni langu la msamaha,” Babu Owino aliandika.
Babu Owino
pia alikariri kuwa bado amepigwa marufuku kutoka Uganda na haruhusiwi kukanyaga
nchini humo.
"Nkienda
Uganda nimepigwa marufuku, siwezi kukanyaga Uganda," alisema.
Serikali ya
Uganda ilimpiga marufuku rasmi mbunge huyo wa Kenya kuingia nchini humo Mei
2019, na kumtangaza kuwa mtu asiyestahili.
Uamuzi huo
ulitokana na kuhusika kwa Babu Owino kumkaribisha Bobi Wine wakati wa ziara
yake nchini Kenya, ambapo wawili hao wanatuhumiwa kutoa matamshi ya uchochezi
dhidi ya utawala wa Museveni.
Mbunge huyo
mkosoaji mkali wa serikali ya rais Ruto alieleza kuwa hakufuatilia sana ya
yaliyomkumba Tanzania, akisisitiza hana sababu ya kutembelea Tanzania.
"Nikienda
Uganda nimepigwa marufuku, siwezi kuingia Uganda. Lakini kusema kweli, je,
nahitaji chochote Tanzania? Ninahitaji nini Tanzania ambacho sipati Kenya?
Sijasafiri hata hela nzima ya Tanzania? Kenya bado ninahitaji nini nchini
Tanzania?"
Babu alisema.