logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nikichaguliwa Sawa Na Nisipichaguliwa Sawa, Si Niko Na Nyumbani Kwetu? - Raila

“Kura itapigwa Jumamosi hii inayokuja, mimi naenda, nikichaguliwa sawa na nisipochaguliwa sawa. Sivyo? Si mimi niko na nyumbani kwetu?” Odinga alisema.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari10 February 2025 - 15:39

Muhtasari


  • Kiongozi huyo wa muda mrefu katika siasa za Kenya pia alisema kwamba hana wasiwasi wowote katika matokeo ya aina yoyote, akiradidi kwamba yuko tayari kwa lolote.
  • “Kwa hiyo mimi nimetoka nimeongea na viongozi wote wa bara la Afrika, wakikubali nitakuwa mwenyekiti wa AU.”

Raila Odinga, mgombea wa uenyekiti wa AUC

KIONGOZI wa chama cha ODM ambaye pia ni mgombea wa wadhifa wa uenyekiti wa bara la Africa, AUC, Raila Odinga ameonyesha utayarifu wake kuelekea uchaguzi huo zikiwa zimesalia siku 4 pekee.

Akizungumza katika mkutano mkuu wa ODM ulioandaliwa katika ukumbi wa Bomas jijini Nairobi leo Jumatatu, Odinga alisema kwamba kujitokeza kwake kuwania kulitokana na msukumo kutoka kwa viongozi wa Afrika.

Odinga alisema kwamba alishawishiwa na baadhi ya viongozi wa Afrika kuwania wadhifa wa uenyekiti wa AUC kwani walimuona kama suluhisho bora kwa matatizo ya bara hili.

“Viongozi wa Afrika waliniambia wananitaka katika Afrika, Afrika iko na shida nyingi zaidi. Wakasema shida ambayo mko nayo Kenya ndio iko Nigeria, Ghana na kwingineko. Kwa hivyo ukija hapa juu tupate suluhisho tutaliweka katika nchi zote za Afrika.”

“Wakaniuliza, ‘kubali uje uwe kama kiongozi wa bara la Afrika’. Nikapiga moyo konde nikajiuliza na Kenya je? Nikasema Kenya iko ndani ya Afrika nan iko tayari kujaribu.”

Odinga alisema ni kutokana na msukumo huo ndio maana ametoka na kukutana na viongozi wote na kusema kwamba kama watakubali basi atakuwa mwenyekiti wa AUC.

Kiongozi huyo wa muda mrefu katika siasa za Kenya pia alisema kwamba hana wasiwasi wowote katika matokeo ya aina yoyote, akiradidi kwamba yuko tayari kwa lolote.

“Kwa hiyo mimi nimetoka nimeongea na viongozi wote wa bara la Afrika, wakikubali nitakuwa mwenyekiti wa AU.”

“Kura itapigwa Jumamosi hii inayokuja, mimi naenda, nikichaguliwa sawa na nisipochaguliwa sawa. Sivyo? Si mimi niko na nyumbani kwetu?” Odinga alisema.

Alimalizia kwa kuwashukuru Wakenya kwa kumuombea na kumtakia mema katika matokeo ya uchaguzi huo utakaofanyika wikendi.

“Ahsanteni sana kwa kuniombea, mimi nitasimama imara na nikienda katika bara la Afrika, nitafanya mambo laini kisawasawa vile nyinyi mnajua tabia yangu,” alisema.

Raila atachuana na Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Djibouti Mahamoud Ali Youssouf na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Madagascar Richard Randriamandrato.

Wadadisi wanasema tishio kubwa la Raila ni mgombeaji wa Djibouti, ambaye anaaminika kuungwa mkono na nchi za Kiislamu na Kiarabu.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved