
MWANAMUME mwenye uraibu wa kucheza michezo ya Kamari amepata pigo mahakamani baada ya ombi lake la kutaka kampuni ya ubashiri ishrutishwe kufunga akaunti yake kukataliwa na mahakama ya juu.
Mwanamume huyo alielekea mahakamani kuishtaki kampuni ya Kamari
akiitaka ishrutishwe kufunga akaunti yake kama njia ya kudhibiti uraibu wake.
Hata hivyo, Jaji Chacha Mwita aligundua kuwa aliwasilisha
malalamiko yake katika mahakama isiyo sahihi.
Kwa mujibu wa gazeti la The Standard, Jaji alisema suala hilo
lilihusisha mkataba, si uvunjaji wa katiba au haki, na hivyo basi, lilipaswa
kuwasilishwa kwenye Mahakama ya Kiraia.
“Baada ya kuzingatia maombi, hoja na maamuzi yanayotegemewa na vyama,
hitimisho ninalofikia ni kwamba hili si hoja ya kikatiba. Masuala yaliyoibuliwa
katika ombi hilo yalitokana na uhusiano wa kimkataba, yanaweza tu kutoa shauri
la madai ikiwa mlalamishi alifikiri kulikuwa na ukiukaji wa sheria inayoongoza
uhusiano huo. Haziwezi kuwa msingi wa malalamiko ya kikatiba,” alisema
Jaji Mwita.
Alidai kuwa alijiandikisha kwa huduma za kamari katika kampuni inayomiliki maduka ya kamari kwa kutumia namba yake ya simu.
Kisha akagundua kwamba alikuwa na tatizo la uraibu wa kamari
na alihitaji kuacha.
Hii ilikuwa mwaka 2020.
Alisema huduma ya wateja wa kampuni ya kamari ilimfahamisha
mnamo Julai 17, 2020 kuacha akaunti ikiwa imelala kwa muda, na itafungwa.
Alisema alisisitiza kuwa akaunti hiyo inapaswa kufungwa mara
moja.
Aidha alisema mwakilishi wa huduma kwa wateja aliomba nakala
ya kitambulisho chake cha taifa ili kuanza mchakato huo.
Hata hivyo, alisema, madai yake hayakuheshimiwa licha ya
simu kadhaa na mawaidha ya barua pepe mnamo Agosti na Septemba mwaka huo.