logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kakamega: Mwanaume ,42, Amuua Kakake, 40, Wakizozania Kiasi Cha Ugali Wangepika

Reuebn Lutaboni mwenye umri wa miaka 42 alizozana na kakake mdogo Michael Lukala mwenye miaka 40 kuhusu kiasi cha ugali ambacho wangestahili kupika.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari20 February 2025 - 08:08

Muhtasari


  • Kwa mujibu wa ripoti, vijana wawili ambao ni kaka wa toka-nitoke walizozania kiasi cha ugali ambacho wangepika kupelekea mmoja wao kuuawa na mwenzake.

Ugali

WAKAAZI wa kijiji cha Kilimani kaunti ya Kakamega waligubikwa na butwaa kufuatia mkasa wa mauaji ya kifamilia.

Kwa mujibu wa ripoti, vijana wawili ambao ni kaka wa toka-nitoke walizozania kiasi cha ugali ambacho wangepika kupelekea mmoja wao kuuawa na mwenzake.

Reuebn Lutaboni mwenye umri wa miaka 42 alizozana na kakake mdogo Michael Lukala mwenye miaka 40 kuhusu kiasi cha ugali ambacho wangestahili kupika wakati Lutaboni alimshambulia mwenzake na kumuua.

“Wawili hawa walikuwa ni marafiki ambao wangefanya vibarua kijijini na walirudi nyumbani kupika chajio wakati mzozo ulipotokea. Mmoja alikuwa anapika wakati mwenzake alimshambulia na shoka kichwani mara kadhaa. Alimgonga kwa ubongo karibu mara 5, upande wa macho akamgonga mara 3 halafu upande wa macho akakata kabisa na kummaliza,” ndugu mkubwa alisema.

Cleophas Barasa, mzee katika kijiji hicho alilaani kitendo hicho huku akitoa wito kwa watu kutatua tofauti zao kwa njia zifaazo kuliko vita.

“Mambo kama haya ya chakula haistahili ndugu kupigana mpaka mwingine anaua mwenzake kwa sababu ya chakula. Watu ambao wako zaidi ya umri wa 40 kuishi pamoja pia ni hatari kwa sababu hujui ni nini kitatokea baadae,” mzee huyo alishauri.

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved