logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mkewe Besigye Atangaza Kuandika Kitabu Kusimulia ‘Urafiki’ Na Museveni Zamani

"Ikiwa ni ya kupendeza kwake, anapaswa kungojea kitabu changu, ni hadithi ya kupendeza!" Byanyima alichapisha kwenye X.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari22 February 2025 - 11:42

Muhtasari


  • Byanyima anaaminika kuwa alikuwa na historia ya kimapenzi na Museveni kabla ya kuolewa na Kizza Besigye mnamo Julai 7, 1999, huko Nsambya, Kampala.
  • Wanandoa hao wana mtoto wa kiume, Anselm Besigye, ambaye kwa sasa anafuata PhD katika Chuo Kikuu cha Columbia huko New York.
Winnie Byanyima, Yoweri museveni

WINNIE Byanyima, mke wa mwanasiasa wa muda mrefu katika siasa za upinzani nchini Uganda Kizza Besigye ametangaza kuwa anaandika kitabu, na sehemu yake itaangazia uhusiano wake wa zamani na Rais Yoweri Museveni.

Byanyima ambaye ni mkurugenzi katika shirika la misaada la Marekani la kupambana na maambukizi ya virusi vya UKIMWI, UNAIDS alisema haya kupitia ukurasa wake wa X alipokuwa akijibu baadhi ya watu wanaojadili kwa njia hasi kuzuiliwa kwa mume wake.

Mwanamke huyo alikuwa akijibu mjadala kwenye NBS TV, ambapo mwanahabari mkongwe Andrew Mwenda aliachana na mada ya madai ya Kizza Besigye kuzuiliwa kinyume cha sheria ili kuanzisha uhusiano wake na Museveni.

Byanyima alimjibu akisema kwamba ikiwa anavutiwa na simulizi ya uhusiano wake wa zamani na Museveni, basi anafaa kusubiri hadi pale yeye [Byanyima] atakapoachilia kitabu chake ili kupata uhondo zaidi.

"Ikiwa ni ya kupendeza kwake, anapaswa kungojea kitabu changu, ni hadithi ya kupendeza!" Byanyima alichapisha kwenye X.

f

Byanyima anaaminika kuwa alikuwa na historia ya kimapenzi na Museveni kabla ya kuolewa na Kizza Besigye mnamo Julai 7, 1999, huko Nsambya, Kampala.

Wanandoa hao wana mtoto wa kiume, Anselm Besigye, ambaye kwa sasa anafuata PhD katika Chuo Kikuu cha Columbia huko New York.

Baadae Ijumaa, Besigye alipata nafuu baada ya kesi yake kuhamishwa kutoka mahakama ya kijeshi hadi katika mahakama ya kiraia ambapo alifunguliwa shtaka la uhaini ambalo adhabu yake ni kifo.

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari, Besigye amekuwa akisusia chakula kwa takribani wiki 2, ishara ya kupinga kufunguliwa mashtaka katika mahakama ya kijeshi sasa amerejelea chakula.

Besigye, mgombea urais mara nne katika nchi hiyo ya Afrika mashariki, alikaa kwenye kiti cha magurudumu alipokuwa akikabiliwa na mashtaka katika chumba cha mahakama katika mji mkuu, Kampala.

Besigye, 68, amekuwa kizuizini tangu Novemba 16, alipotoweka katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi.

Siku kadhaa baadaye, alifikishwa mbele ya mahakama ya kijeshi mjini Kampala kujibu mashtaka ya kutishia usalama wa taifa.

Mahakama ya Juu ilisimamisha kesi yake ya kijeshi mwezi uliopita, ikisema jopo la mahakama ya kijeshi haliwezi kuwahukumu raia.

Familia ya Besigye, wafuasi na wengine walitaka aachiliwe mara moja, lakini aliwekwa katika gereza lenye ulinzi mkali na baadaye kuanza mgomo wa kula.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved