logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Alai Ataka Orengo Na Nyong’o ‘Kufa’ Kisiasa Kwa Kutosaidia Wajaluo Licha Ya Kuwa Wanarika Na Raila

Alisema kwamba ni wakati umefika wawili hao ‘kufa na kuzikwa’ kisiasa ili kutoa nafasi kwa viongozi wachanga wenye maoni kuhudumia watu wa Luo Nyanza na kuwaokoa kutoka taabu na umaskini.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari23 February 2025 - 11:27

Muhtasari


  • Aidha, malalamishi yake hayakumsaza katibu mkuu wa ODM Edwin Sifuna ambaye baadhi ya wanachama wanahisi anatumika kisiasa na aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua.
  • Tetesi za Sifuna kuvutia upande wa Gachagua kisiasa ziliibuliwa na George Aladwa, mbunge wa Makadara ambaye pia ni mwenyekiti wa chama hicho tawi la Nairobi.
Robert Alai

MWAKILISHI wadi wa Kileleshwa, Robert Alai amewataka vigogo wa chama cha ODM, gavana wa Siaya James Orengo na mwenzake wa Kisumu Anyang’ Nyong’o kujiondoa katika siasa za eneo la Luo Nyanza akidai kwamba hakuna lolote la maana wamewahi fanya.

Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Alai alisema kwamba Orengo mwenye umri wa miaka 74 na Nyong’o mwenye miaka 79 ni wanarika na kiongozi wa ODM Raila Odinga lakini athari yao kimaendeleo ni finyu mno ikilinganishwa na Odinga mwenyewe.

Alisema kwamba ni wakati umefika wawili hao ‘kufa na kuzikwa’ kisiasa ili kutoa nafasi kwa viongozi wachanga wenye maoni kuhudumia watu wa Luo Nyanza na kuwaokoa kutoka taabu na umaskini.

“Nyongo na Orengo wana umri wa miaka 79 na 74 mtawalia. Ni wanarika wa Raila Amolo Odinga. Hawatakuonyesha jambo lolote la maana walilofanya kuwainua vijana wa Kijaluo kutoka katika taabu na umaskini. James Orengo na Anyang Nyong'o lazima wafe kisiasa mara moja na wazikwe. Sioni thamani katika siasa zao!,” Alai alisema.

MCA huyo aliendelea kuwalaumu wawili hao kwa kile alidai kwamba kazi yao imekuwa ni kuwatumia vijana Wajaluo kwa maandamano kwa faida zao wenyewe, akisema kuwa bila Raila Odinga, wote hawako.

“Wameishi maisha ambayo wanajua tu kupeleka vijana wa Kijaluo kufia mitaani ili hata mabilioni yao yaongezeke. Orengo na Nyong'o wananing'inia kwenye koti la Raila wakiwa na wazo gumu sana la nini Wajaluo wanapaswa kufanya ili kufa kwa ajili ya Kenya na kuleta mabadiliko ya kimawazo ambayo wao wenyewe wameyapata.”

“Leo ukiuliza Orengo au Nyong'o ni nani mbadala wao kutoka kwa Ruto, hawatafikiria zaidi ya Baba Raila Odinga. Hawana wazo! Hawana fununu ya kile ambacho watu wanapaswa kufanya ili kufikia nirvana wanayofikiria,” Alai aliongeza.

alai

Aidha, malalamishi yake hayakumsaza katibu mkuu wa ODM Edwin Sifuna ambaye baadhi ya wanachama wanahisi anatumika kisiasa na aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua.

Tetesi za Sifuna kuvutia upande wa Gachagua kisiasa ziliibuliwa na George Aladwa, mbunge wa Makadara ambaye pia ni mwenyekiti wa chama hicho tawi la Nairobi.

Aladwa alimuonya Sifuna kwamba huenda hivi karibuni akatimuliwa kama katibu wa ODM kama ambavyo mtangulizi wake Ababu Namwamba alivyofanyiwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved