logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nataka urais ndio niweze kutunza Kenya kama vile mama anatunza boma – Martha Karua

“Keki ya Kenya tunataka igawe kwa usawa, sio vile ilivyo siku hizi. Mmejaribu wanaume huo wakati wote lakini safari hii nawaomba mjaribu mama kupitia PLP,” Karua alirai wananchi.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari22 April 2025 - 12:49

Muhtasari


  • Alisema kwamba Kenya ina utajiri wa kipekee ambao unafaa kumfaidi kila mwananchi, akionekana kuashiria kwamba ilivyo kwa sasa, kuna upendeleo katika ugavi wa raslimali za taifa.
  • “Keki ya Kenya tunataka igawe kwa usawa, sio vile ilivyo siku hizi. Mmejaribu wanaume huo wakati wote lakini safari hii nawaomba mjaribu mama kupitia PLP,” Karua alirai wananchi.

Martha Karua

KIONGOZI wa chama cha People’s Liberation Party, PLP Martha Karua amedokeza kwamba ni wakati sasa Kenya kuongozwa na rais mwanamke.

Akizungumza Jumatatu katika kaunti ya Isiolo, Karua aliweka wazi nia yake ya kuwania urais, akisema kwamba atalitunza taifa la Kenya kwa njia sahihi ya upendo kama jinsi ambavyo mama hutunza boma lake.

“Kile kiti mimi nataka ni cha urais. Na ndivyo kama mama niweze kutunza Kenya vile ambavyo mama hutunza boma. Mama hawezi kuacha mtoto hata mmoja kulala njaa. Hata chakula kikiwa kidogo mama anagawa kidog-kidogo ili kila mmoja apate, hata mtu wa kupita anapatiwa yake kidogo,” Martha Karua alisema.

Kiongozi huyo ambaye tangu kusambaratika kwa uliokuwa muungano wa upinzani wa Azimio amekuwa akiikosoa serikali mara kwa mara amekuwa akionekana kuweka hai matumaini yake ya kuliongoza taifa.

Alisema kwamba Kenya ina utajiri wa kipekee ambao unafaa kumfaidi kila mwananchi, akionekana kuashiria kwamba ilivyo kwa sasa, kuna upendeleo katika ugavi wa raslimali za taifa.

“Keki ya Kenya tunataka igawe kwa usawa, sio vile ilivyo siku hizi. Mmejaribu wanaume huo wakati wote lakini safari hii nawaomba mjaribu mama kupitia PLP,” Karua alirai wananchi.

Karua ameonekana kukubali Ushirikiano na viongozi wengine wa upinzani akiwemo aliyekuwa naibu wa rais Rigathi Gachagua na Kalonzo Musyoka katika kuzindua muungano dhabiti wa kushindana na rais Ruto katika uchaguzi wa urais 2027.

Cha ajabu ni kwamba licha ya viongozi hao wote kuonekana kuwa na nia ya kufanya kazi pamoja, kila mmoja wake kwa wakati wake amekuwa akiweka wazi kwamba atawania urais 2027.

 

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved