Kiongozi wa chama cha Democracy for Citizen Party (DCP) na aliyekuwa Naibu Rais, Rigathi Gachagua, amewataka wakazi wa Meru kususia hoteli moja ya kifahari ambayo anadai inahusiana na Rais William Ruto.
Akizungumza katika Kaunti ya Meru mwanzoni mwa ziara yake ya siku tatu katika eneo hilo siku ya Ijumaa, Gachagua alidai kuwa Rais alikuwa akijenga barabara kuelekea hoteli yake mpya huko Meru.
Ijumaa, Gachagua alimtuhumu Rais kwa kumng’oa madarakani kwa misingi ya madai ya uongo, yakiwemo yale yanayohusu ununuzi tata wa kipande cha ardhi katika Kaunti ya Meru.
Kiongozi huyo wa DCP pia aliwakosoa baadhi ya Wabunge ambao aliwatuhumu kwa kushirikiana katika mchakato wa kumuondoa ofisini, hatua ambayo anadai imekosesha eneo hilo fursa muhimu za maendeleo.
"Mimi singekubali kuungana naye akiuwa watoto. Alitaka kugawanya Mlima ndio atukalie vile Moi alitukalia kwa miaka 24. Alitaka kutumia huyu soprano eti Wameru, Wakikuyu na Waembu wagawane ndio atutawale," he said.
"Nguvu yetu ni kukaa tukiwa pamoja. Sasa wewe Kasongo, badala utujengee barabara ya kutupelekea mazao kwa factoria, wewe unajenga barabara ya kuenda kwa hoteli yako, na unafikiria Wameru ni wajinga watakuja kukunywa chai katika hoteli yako... Kasongo anyolewe, asinyolewe."