logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gachagua Anyeshewa na Mawe na Marungu Bungoma

Gachagua alichapisha picha za sehemu ya msafara wake ulioharibiwa na watu wasiojulikana waliokuwa wamejihami kwa marungu, mawe na silaha nyingine hatari katika eneo la Chwele.

image
na Tony Mballa

Habari04 July 2025 - 18:57

Muhtasari


  • Akihutubia halaiki mnamo Ijumaa, Juni 4, 2025, katika mkutano wa hadhara Busia kama sehemu ya hitimisho la ziara ya Muungano wa Loyal Opposition Ukanda wa Magharibi, Gachagua aliwaambia wananchi kuwa jamii ya Waluhya “imekuwa ikidhulumiwa na kutupiliwa mbali mara kwa mara” na Raila kwa miongo kadhaa.
  • Aliukosoa vikali mtindo wa Raila wa kuingia serikalini kupitia siasa za handisheki baada ya uchaguzi, akisema kuwa kila mara anapoungana na serikali, wapiga kura wa eneo la Magharibi huachwa upinzani bila manufaa ya moja kwa moja.

Aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua alipigwa mawe akiwa katika eneo hilo akiendeleza kampeni ya kuwaunga mkono viongozi wa Muungano wa Upinzani wa Kitaifa kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika baada ya miaka miwili.

Gachagua alichapisha picha za sehemu ya msafara wake ulioharibiwa na watu wasiojulikana waliokuwa wamejihami kwa marungu, mawe na silaha nyingine hatari katika eneo la Chwele.

Gari la Gachagua lililomiminiwa mawe Bungoma

Kupitia taarifa rasmi, Gachagua alisema kuwa vurugu hazina nafasi katika taifa, na kwamba viongozi wanaotumia ukatili wanadhoofisha misingi ya utawala bora na demokrasia ya kweli.

“Watu wa Eneobunge la Kimilili katika Kaunti ya Bungoma wamezungumza kwa sauti kubwa na wazi: vurugu na mauaji ya kiholela hayana nafasi katika jamii yetu. Serikali zinazostawi kwa misingi ya ukatili hudumu kwa muda mfupi na hazina uhalali,” Gachagua alisema.

“Lazima tukemee vitendo kama hivyo popote vinapotokea na tusimame imara dhidi yake. Amani, haki na kuheshimu haki za binadamu ndizo nguzo za jamii yenye maendeleo,” aliongeza.

Gari la Gachagua lililomiminiwa mawe Bungoma

Akihutubia halaiki mnamo Ijumaa, Juni 4, 2025, katika mkutano wa hadhara Busia kama sehemu ya hitimisho la ziara ya Muungano wa Loyal Opposition Ukanda wa Magharibi, Gachagua aliwaambia wananchi kuwa jamii ya Waluhya “imekuwa ikidhulumiwa na kutupiliwa mbali mara kwa mara” na Raila kwa miongo kadhaa.

Aliukosoa vikali mtindo wa Raila wa kuingia serikalini kupitia siasa za handisheki baada ya uchaguzi, akisema kuwa kila mara anapoungana na serikali, wapiga kura wa eneo la Magharibi huachwa upinzani bila manufaa ya moja kwa moja.

Gachagua, ambaye kwa sasa ni kiongozi wa chama cha Democracy for Citizens Party (DCP), alisema kuwa eneo la Mlima Kenya pia limekumbwa na hali kama hiyo chini ya uongozi wa Rais William Ruto.

“Sisi wa Mlima Kenya pia tumetumika kisha kutupwa,” alisema. “Ruto alituahidi maendeleo lakini alituletea usaliti.”

Haya yanajiri siku moja tu baada ya Gachagua kudai kuwa ameweza kulinda eneo la Mlima Kenya dhidi ya ushawishi wa Rais Ruto, na kwamba yeye ndiye mwenye funguo.

“Nilikua naibu wa Ruto, je, mnamjua kuliko mimi? Je, mtatupa viongozi wenu ili tukubaliane namna ya kuchukua uongozi wa nchi hii? Huko Mlima Kenya nilimfungia Ruto nje, na funguo ninazo, nazibeba kila mahali ninaenda,” Gachagua alisema.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved