logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Aliyekuwa mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati aaga dunia baada ya kuugua kwa muda

Chebukati alihudumu kama mwenyekiti wa IEBC kwa muhula mzima wa miaka sita na alistaafu Januari 2023.

image
na Davis Ojiambo

Hivi Punde21 February 2025 - 08:59

Muhtasari


  • Chebukati alihudumu kama mwenyekiti wa IEBC kwa muhula mzima wa miaka sita na alistaafu Januari 2023.

Aliyekuwa mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) Wafula Chebukati ameaga dunia.

Chebukati alifariki akipokea matibabu katika hospitali moja mjini Nairobi.

Chebukati alikuwa melazwa katika hospitali moja jijini Nairobi ambapo amekuwa akitibiwa kwa takriban wiki moja.

Duru kutoka hospitali zilikuwa zimesema kwamba alikuwa amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi katika hospitali hiyo.

Chebukati alihudumu kama mwenyekiti wa IEBC kwa muhula mzima wa miaka sita na alistaafu Januari 2023.

Aliongoza chaguzi za 2017 na 2022.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved