logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tanzania: Kiongozi wa upinzani ataka Rais Samia kueleza ukweli kuhusu jaribio la mauaji

.Lissu alifanyiwa upusuaji kwa mara ya  25 baada ya kupigwa  marisasi 16 yaliyompata kwenye miguu, mikono na kwenye tumbo mwakani 2017

image
na Radio Jambo

Makala09 June 2021 - 03:31

Muhtasari


•Baada ya hayo kutukia, Lissu alienda mafichoni nchini Ubelgiji na kurudi Tanzania miaka tatu baadae ili kuwania kiti cha Urais. 

•Lissu amemtaka Rais Samia kueleza tukio hilo kuona kuwa kwa wakati ule alikuwa naibu rais kwenye serikali ya Rais Magufuli.

Tundu Lissu Hospitalini

Kiongozi wa upinzani nchini Tanzania, Tundu Antiphas Lissu amemuagiza Rais Samia Suluhu kueleza taifa ukweli kuhusu nani aliyekuwa ameamuru kuuliwa kwake na kwa nini.

Alipokuwa anatangaza mafanikio katika upasuaji wake wa mara ya 25 siku ya Jumanne, kufuatia jaribio la mauaji lililofanyika miaka minne iliyopita, Lissu alisema kuwa kimya cha Rais Samia kinahofisha.

"Leo nimefanyiwa upasuaji wa mara ya 25 kufuatia jaribio la mauji lililofanyika tarehe Septemba 7, 2017. Huku Magufuli akiwa ameenda, ni wakati rais mpya Samia aniambie na aambie taifa ni nani aliyekuwa nyuma ya kupigwa marisasi kwangu na kwa nini? nani alipeana amri? Kimya chake hakiwezi vumiliwa tena!" Lissu aliandika kwenye mtandao wa Twitter.

Katika tukio hilo, Lissu alivamiwa na kikundi cha wauaji wawili waliopiga gari lake marisasi alipokuwa anawasiri nyumbani kwake akitokea kwenye kikao cha bunge mjini Dodoma.

Lissu alipokea marisasi 16 yaliyompata kwenye miguu, mikono na kwenye tumbo. Hata hivyo, alinusurika na kupelekwa katika hospitali ya Aghakan nchini Kenya ambako alipokea matibabu.

Mwanasiasa huyo ambaye aliwania kiti cha urais nchini Tanzania mwaka uliopita bila mafanikio alilaumu serikali kwa jaribio hilo huku akisema kuwa siku hiyo walinzi walikuwa wameondolewa kwenye boma lake ili kufanikisha mauaji hayo. Kwa wakati huo Lissu alikuwa kiranja wa wapinzani katika bunge la kitaifa.

Baada ya hayo kutukia, Lissu alienda mafichoni nchini Ubelgiji na kurudi Tanzania miaka tatu baadae ili kuwania kiti cha Urais. Hata hivyo, alibwagwa chini na Hayati Rais Magufuli aliyega mapema mwakani.

Lissu amemtaka Rais Samia kueleza tukio hilo kuona kuwa kwa wakati ule alikuwa naibu rais kwenye serikali ya Rais Magufuli.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved