logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Tunampenda kijana wetu mzuri na tutampeza milele" Biden aomboleza mbwa wake kwa ujumbe maalum

Amesema kuwa 'Champ', kama alivyoitwa mbwa yule, hakuwa mbwa wa kawaida tu ila alikuwa mwenzao waliyempenda sana

image
na Radio Jambo

Habari20 June 2021 - 03:29

Muhtasari


•"Amekuwa mwenzetu daima kwa kipindi cha miaka kumi na mitatu iliyopita na alipendwa na familia yote ya Biden. Hata nguvu yake ilipoendelea kudidimia miezi ya hivi karibuni, tulipoingia kwa nyumba alikuwa anajiinua huku akitingisha mkia na kutaka tumsugue sikio ama tumbo" Biden aliandika.

•Champ alikuwa mmoja kati ya mbwa wawili wa rais Biden wanaojulikana na alikuwa ndiye mkubwa kati ya mbwa hao wawili

Biden na mbwa wake 'Champ'

"Nyoyo zetu ni nzito siku ya leo tunapowajulisha nyote kuwa mbwa wetu aina ya German Shepherd tuliyempenda zaidi ameaga kwa amani hapa nyumbani" ndio ujumbe ambao aliandika rais wa Marekani Joe Biden siku ya Jumamosi.

Rais Biden ameandika ujumbe maalum akimsfia na kuomboleza mbwa ambaye amekuwa akiishi na familia yake kwa kipindi cha miaka kumi na mitatu.

Amesema kuwa 'Champ', kama alivyoitwa mbwa yule, hakuwa mbwa wa kawaida tu ila alikuwa mwenzao waliyempenda sana.

"Amekuwa mwenzetu daima kwa kipindi cha miaka kumi na mitatu iliyopita na alipendwa na familia yote ya Biden. Hata nguvu yake ilipoendelea kudidimia miezi ya hivi karibuni, tulipoingia kwa nyumba alikuwa anajiinua huku akitingisha mkia na kutaka tumsugue sikio ama tumbo" Biden aliandika.

Champ

Amesema kuwa Champ alipendelea sana kuwa mahala popote ambapo walikuwa.

"Alipenda zaidi kujikunja kwenye miguu yetu mbele ya moto kila jioni, tuungana nasi kwenye mikutano ama kuota jua kwenye shamba la ikulu.  Kwenye siku zetu za furaha na  zile za huzuni, alikuwa hapo nasi, ni ngumu kueleza hisia fiche zilizo ndani ya nyoyo zetu kwa sasa. Tunampenda kijana wetu mzuri na tutampeza milele" aliandika rais Biden.

Champ alikuwa mmoja kati ya mbwa wawili wa rais Biden wanaojulikana . Alikuwa ndiye mkubwa kati ya mbwa hao wawili

Major ambaye ndiye mbwa wa pili wa Biden alizaliwa mwaka wa 2018.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved