logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais wa Malawi amvua naibu mamlaka juu ya ufisadi

Katiba ya Malawi hairuhusu rais kumfukuza kazi makamu wake kwa vile ni afisa aliyechaguliwa.

image
na Radio Jambo

Habari22 June 2022 - 08:47

Muhtasari


• Hii ni kuhusiana na kandarasi 16 ambazo Huduma ya Polisi ya Malawi na Jeshi la Ulinzi la Malawi zilitoa kwa kampuni tano za Bw Sattar.

• Makamu wa rais bado hajajibu tuhuma hizo.

• Bw Chakwera aliungana na Bw Chilima kumshinda Peter Mutharika katika uchaguzi wa urais wa 2020.

Rais wa Malawi Lazarus Chakwera amemvua makamu wake Saulos Chilima mamlaka yote aliyokabidhiwa baada ya kutajwa katika kashfa ya ufisadi ya $150m (£123m) iliyohusisha kandarasi za serikali.

Makamu wa rais bado hajajibu tuhuma hizo.

Ripoti ya Taasisi ya Kupambana na Rushwa nchini (ACB) iliwataja maafisa 53 wa sasa na wa zamani kuwa walipokea pesa kutoka kwa mfanyabiashara kutoka Uingereza na Malawi Zuneth Sattar kati ya 2017 na 2021, rais alisema.

Hii ni kuhusiana na kandarasi 16 ambazo Huduma ya Polisi ya Malawi na Jeshi la Ulinzi la Malawi zilitoa kwa kampuni tano za Bw Sattar.

Maafisa waliotajwa kwenye ripoti hiyo ni pamoja na makamu wa rais na mkuu wa polisi - ambaye amefutwa kazi.

Lakini sheria ya Malawi hairuhusu rais kumfukuza kazi au kumsimamisha kazi makamu wake kwa vile rais huyo ni afisa aliyechaguliwa.

"Kila bora ninachoweza kufanya kwa sasa, ambacho nimeamua kufanya, ni kunyima afisi yake majukumu yoyote aliyokabidhiwa huku nikisubiri ofisi ithibitishe madai dhidi yake," rais alisema katika hotuba ya kitaifa Jumanne.

Bw Chakwera aliungana na Bw Chilima kumshinda Peter Mutharika katika uchaguzi wa urais wa 2020. Wawili hao walikuwa wameahidi kupambana na ufisadi serikalini.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved