logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mbunge ashauri kuanzishwa kwa viwanda vya kupunguza makali ya bangi kabla kutumiwa

"Tuweze kujenga viwanda ambavyo vitapunguza makali ili bangi hii iweze kutumika kwenye maeneo mbali mbali" - Ngonyani.

image
na Radio Jambo

Kimataifa14 September 2022 - 12:17

Muhtasari


• Wako watu wakitumia hivyo wanaweza kulima zaidi, anaweza kufanya kazi hii na mwingine anavuta tu kama sigara - Ngonyani.

Mbunge maalum ataka serikali kuhalalisha bangi

Mbunge maalumu nchini Tanzania amepeleka bungeni suala la kutaka serikali ya nchi hiyo kuanzisha ujenzi wa viwanda vya bangi.

Mbunge huyo maalumu kwa jina Jackline Ngonyani alizungumza kwenye bunge akitaka serikali kuanzisha mchakato na kuwepo kwa viwanda hivyo vitakavyofanay kazi ya kuchukua bangi na kuipunguza makali kabla ya kuwapa wananchi kuitumia kadri wanavyojihisi.

Akitetea hoja yake, mbunge Ngonyani alisema kwamba nchini humo wapo watu wengi ambao wanapanda na kutumia bangi pasi na serikali kujua kwa sababu haina mifumo ya kuweza kujua mtu fulani amepanda bangi na kusema ni wakati wananchi waruhusiwe kuitumia pindi tu inapopunguzwa makali.

“Suala la bangi mimi ndio naona tatizo kubwa sana, kwa sababu bangi inalimwa hata kwenye upenuni mwa nyumba, hata bafuni mtu anaweza akalima bangi hiyo na mwisho wa siku anaitumia kimya kimya. Hatuna mifumo ya kujua nyumba hii au shamba hili lina bangi,” mbunge huyo alisema.

“Sasa basi kwa nini suala hili la bangi tusilichukue tukakaa upya tukajadiliana ili ikiwezekana bangi hii tuiprocess, na tuweze kujenga viwanda ambavyo vitapunguza makali ili bangi hii iweze kutumika kwenye maeneo mbali mbali kwa sababu wako watu wakitumia hivyo wanaweza kulima zaidi, anaweza kufanya kazi hii na mwingine anavuta tu kama sigara,” mbunge Ngonyani alitetea hoja yake kwa msisitizo.

Hakuishia hapo. Mbunge huyo alijihami vizuri na mifano hai ambapo alisema nchi kama Zimbabwe wanalima bangi na tayari wameshaipitisha kaam biashara ya kuingiza pato la taifa.

Mifano mingine aliyotolea ni Jamaica, Marekani, Korea Kaskazini na kusema nchi kama Tanzania kwani wanakwama wapi badala ya kukumbatia ukulima huu wa kuzalisha pato la taifa.

“Kwa nini sisi tusiiprocess tukapunguza makali na watu watumie kama kadri mtu anavyoona sawa sawa na sigara wanasema tumia lakini ni hatari kwa afya yako. Kwa hiyo mtu ana hiari kuitumia au kuiacha kuliko kuacha pato hili la taifa linaendelea kutokomea,” mbunge huyo alisema huku bunge zima zikipasuka vicheko.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved