logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanafunzi wa umri wa miaka 17 ajifyatulia risasi, aacha barua mwili wake uchomwe

Alitumia bastola ya mtu kwa jina Boniface Kimario ambayo jeshi la polisi lilidhibitisha ni mmiliki halali ila kwa sasa naye ameshikiliwa kwa uchunguzi zaidi.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri15 September 2022 - 10:26

Muhtasari


 
• Kwa mujibu wa Kamanda Maigwa, baba yake Robert alifariki dunia akiwa Marekani na mwili wake haukusafirishwa Tanzania kwa ajili ya maziko bali ulizikwa huko ughaibuni.

Mwanafunzi ajiua kwa kujipiga risasi Kilimanjaro

Mwanafunzi wa umri wa miaka 17 amejiua kwa kujipiga risasi na kisha kuacha maagizo kwamba mwili wake usizikwe bali uchomwe.

Tukio hili liliripotiwa nchini Tanzania katika mkoa wa Kilimanjaro. Mwanafunzi huyo kwa jina Robert Meier alikuwa anasoma kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari St Mary Goreti iliyopo Manispaa ya Moshi mkoani humo.

Kulingana na taarifa zilizosambazwa na Mwananchi Digital, kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa alithibitisha kutokea kwa tukio hilo akisema lilitokea usiku wa kuamkia juzi.

Maigwa alidai kuwa kabla ya mwanafunzi huyo kujiua, aliacha ujumbe wa maandishi ulisomeka mwili wake uchomwe na majivu yake yasafirishwe kwenda Marekani yakazikwe pembezoni mwa kaburi la baba yake.

Kwa mujibu wa Kamanda Maigwa, baba yake Robert alifariki dunia akiwa Marekani na mwili wake haukusafirishwa Tanzania kwa ajili ya maziko bali ulizikwa huko ughaibuni.

Mwanafunzi huyo alijifyatulia risasi katika upande wa kushoto wa kifua kwenye moyo na kutokea mgongoni. Alitumia bastola ya mkaazi mmoja wa maeneo hayo kwa jina Boniface Kimario ambayo jeshi la polisi lilidhibitisha ni mmiliki halali ila kwa sasa naye ameshikiliwa kwa uchunguzi zaidi.

Hayo yanajiri katika nchi Jirani miezi michache tu baada ya humu nchini mtoto wa mbunge maalumu David Ole Sankok kujiua kwa kujifyatulia risasi nyumbani kwao katika kaunti ya Narok.

Mtoto huyo wa kiume mwenye umri wa miaka 15 alikuwa pia ni mwanafunzo katika shule ya upili ya Kericho.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved