Njia chungu ambayo mwanablogu maarufu wa Meru alifariki hatimaye yabainika

Marehemu alinyongwa shingoni, kulingana na uchunguzi wa maiti uliofanyika kwenye mwili wake siku ya Ijumaa.

Muhtasari

•Mwanapatholojia alifanya uchunguzi huo katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Hospitali ya Marimanti Level 4 siku ya Ijumaa.

•Marehemu alikuwa na majeraha kwenye fuvu la kichwa na kuvunjika mbavu, jambo lililodokeza kuwa alinyongwa kabla ya kutupwa mtoni.

Marehemu Daniel Muthiani,
Image: HISANI

Uchunguzi wa maiti umebaini kuwa mwanablogu Daniel Muthiani, ambaye pia anajulikana kama Sniper, alinyongwa hadi kufa.

Marehemu alikuwa na makazi yake Meru.

Alinyongwa shingoni, kulingana na uchunguzi wa maiti uliofanyika kwenye mwili wake siku ya Ijumaa.

Johansen Oduor, mwanapatholojia wa serikali, alifanya uchunguzi huo katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Hospitali ya Marimanti Level 4 siku ya Ijumaa.

Kulingana na Oduor, Sniper alikuwa na alama kwenye shingo yake na alionyesha dalili za kukosa hewa ya oksijeni.

Isitoshe, alikuwa na majeraha kwenye fuvu la kichwa na kuvunjika mbavu, jambo lililodokeza kuwa alinyongwa kabla ya kutupwa mtoni.

Kwa kuwa mwili wake ulikuwa tayari umeoza, maafisa walikusanya sampuli za DNA ili kuthibitisha kuwa yeye ndiye.

Kulikuwa na mashaka juu ya iwapo alikuwa amezidiwa kiasi kwamba alishindwa kujikinga baada ya ukaguzi wa mwili kubaini kuwa hakuna jeraha lililoambatana na kujilinda.

Mwanapatholijia alithibitisha ukweli kwamba vipande vya mwili wa Sniper vilibaki mzima.

Wanafamilia walionyesha kuridhishwa na uchunguzi huo na kuvitaka vyombo vya sheria kuwakamata waliohusika ili haki itendeke.

Kabla ya mwili wake kupatikana mnamo Desemba 16, 2023, Sniper alitoweka mnamo Desemba 2.

Kulingana na vyanzo vya polisi, washukiwa wa mauaji hayo wametambuliwa. Miongoni mwao ni wafanyakazi wachache wa ndani.