logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Watu 4 wafariki, kadhaa wajeruhiwa baada ya gari la mashindano kuwagonga watazamaji

Video kwenye mitandao zilionyesha gari likipoteza mvuto kwenye barabara ya lami kabla ya kuteleza na kuwaingia watazamaji.

image
na Radio Jambo

Habari25 March 2024 - 07:31

Muhtasari


  • Video kwenye mitandao ya kijamii zilionyesha gari likipoteza mwelekeo wenye barabara ya lami kabla ya kuteleza na kuwaingia watazamaji waliokuwa wamekusanyika kutazama mbio hizo.

Watu wanne waliuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa siku ya Jumapili wakati dereva aliyekuwa akishiriki katika mashindano ya magari yawa Hungary Motorsport alipotoka barabarani na kuwagonga watazamaji.

Kulingana na taarifa ya polisi, bado haijabainika ni kwa nini gari lililokuwa likishiriki katika Mashindano ya siku mbili ya Esztergom Nyerges katika eneo la kaskazini mwa Hungary liliacha njia yake.

Ajali hiyo ilitokea kati ya miji ya Labatlan na Bajot kaskazini mwa kaunti ya Komarom Esztergom, na kuacha takriban watu 4 wakiwa wamekufa na saba kujeruhiwa, Polisi walisema na kuongeza kuwa uchunguzi unaendelea.

Ambulensi kadhaa na helikopta za uokoaji zilitumwa kwenye eneo la tukio, na mashindano hayo ulisitishwa mara moja.

Video kwenye mitandao ya kijamii zilionyesha gari likipoteza mwelekeo kwenye barabara ya lami kabla ya kuteleza na kuwagonga watazamaji waliokuwa wamekusanyika kutazama mbio hizo. 

Chama cha Kitaifa cha Michezo cha Hungary (MNASZ) kilitoa rambirambi kwa jamaa na wanafamilia wa wahasiriwa.

Iliapa kushirikiana na mamlaka kuchunguza mazingira ya ajali hiyo bila kuchelewa.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved