'Mungu alikuwa upande wangu' - Trump aelezea jaribio la kumuua

"Kama singesogeza kichwa changu mara ya mwisho, risasi ya muuaji ingefikia lengo lake" alisema.

Muhtasari

• “Nasimama mbele yenu katika uwanja huu tu kwa neema ya Mwenyezi Mungu. Watu wengi wanasema ilikuwa wakati mzuri," alisema.

Image: BBC

"Kulikuwa na damu iliyomwagika kila mahali, na hata hivyo, kwa namna fulani nilijisikia salama sana, kwa sababu nilikuwa na Mungu upande wangu," Trump anasema, wakati anaendelea kuelezea kilichotokea wakati wa shambulio dhidi yake.

"Kama singesogeza kichwa changu mara ya mwisho, risasi ya muuaji ingefikia lengo lake , na nisingekuwa nanyi usiku wa leo."

"Sitakiwi kuwa hapa usiku wa leo," anasema. “Nasimama mbele yenu katika uwanja huu tu kwa neema ya Mwenyezi Mungu. Watu wengi wanasema ilikuwa wakati mzuri."

Tumesikia baadhi ya marejeleo ya kuingilia kati kwa Mungu katika kongamano la wiki hii wakati wazungumzaji wamekuwa wakijadili jaribio la kumuua rais huyo wa zamani , na Trump anagusia mada hiyo tena