logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Boeng inajenga ndege 2 mpya za Air Force One inayotarajiwa kukamilika mwakani

Ndege hiyo ina chumba cha rais, chumba cha mamkuli na chumba cha mikutano, duka la dawa, vifaa vya matibabu ya dharura

image
na Brandon Asiema

Kimataifa10 January 2025 - 15:34

Muhtasari


  • Air Force One ni ndege maalum inayotumiwa na marais wa Marekani.
  • Kampuni ya Boeng pia imechangia dola milioni moja (Ksh 129.45) kwa ajili ya shughuli ya uapisho wa rais mteule .


Kampuni ya anga inayounda, kutengeneza na kuhudumia ndege za kibiashara na kijeshi ya Boeng inaendelea na utengenezaji wa ndege maalum inayotumika na rais wa Marekani maarufu kama Air Force One ambayo inatarajiwa kuanza kutumika na rais mteule Donald Trump baada ya kumalizika kutengenezwa.

Mnamo Februari mwaka 2018, katika muhula wake wa kwanza uongozini, Donald Trump na kampuni ya Boeng waliafikiana kutengenezwa kwa ndege mbili za Air Force One ambazo ziligharimu dola bilioni 3.9 (sawia na shillingi bilioni 504.855). Ndege hizo zilistahili kukamilika kufikia mwaka wa 2021.

Hata hivyo kampuni hiyo inaendelea na ujenzi wa ndege hizo mbili na zinatarajiwa kukamilika mwaka ujao. Hii ni kwa mujibu wa chombo cha habari cha kimataifa cha BBC.

Kampuni ya Boeng pia imechangia dola milioni moja (Ksh 129.45) kwa ajili ya shughuli ya uapisho wa rais mteule         Donald Trump utakaofanyika tarehe 20, Januari mwaka huu.

Boeng imejiunga na kampuni nyingine ikiwemo Google, Meta, Chevron, Ford, Toyota, General Motors na nyingine kutoa pesa kwa kamati ya uapisho wa rais Donald Trump kuingia ikulu ya White House.

Ndege ya Air Force One ni ya kipekee ambayo huyumiwa na marais wa Marekani. Ndege hiyo aina ya Boeng 747-200B kwa jina lingine VC-25 ina vigezo vya hali ya juu.

Ndege hiyo ina chumba cha rais, chumba cha mamkuli na chumba cha mikutano, duka la dawa, vifaa vya matibabu ya dharura, na gali. Pia ndegeg hiyo inaweza kuongezwa mafuta ikiwa angani wakati wa dharura.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved