logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Seneta Murkomen asherehekea BBI kuaguka

Seneta Murkomen ameonyesha furaha yakle baada ya mahakama ya upeo kutupilia mbali mswada wa BBI.

image
na Radio Jambo

Habari31 March 2022 - 12:27

Muhtasari


• meshikilia kwamba BBI haikufuata sheria a hivyo ilipaswa kuangushwa.

• "Haikuwa sawa kisheria, narudia haikuwa sawa kisheria," Murkomen aliandika.

Seneta wa kaunti ya Elgeyo Marakwet, Kipchumba Murkomen ameonyesha furaha yake baada ya mswada wa BBI kutupiliwa mbali na mahakama ya upeo.

Kupitia ujumbe alioandika katika ukurasa wake wa Facebook, Murkomen alisema kwamba mswada huo haustahiki kabisa kuidhinishwa na unapaswa kukataliwa kwa hali hali zote.

"Haikuwa sawa kisheria, narudia haikuwa sawa kisheria," Murkomen aliandika.

Murkome ni moja kati ya viongozi waliopo katika chama cha UDA ambao wamekuwa wakipinga vikali kuidhinishwa kwa mswada huo wa BBI kuwa sheria.

Viongozi waaogemea upande wa naibu rais William Ruto, walikuwa wakipinga mchakato huo wa kuifanyia katiba marekebisho kwa kile walikitaja kuwa, mswada huo ulikuwa unalenga kuwanufaisha viongozi wachache serikali na kuwaacha wananchi wakihangaika.

Kupitia kwa jaji mkuu Martha Koome, mahakama ya upeo ilisema kwamba rais Uhuru Kenyatta hakuwa na uwezo kisheria kuasisi mchakato wa kuifanyia katiba mabadiliko.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved