logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Baba aua bintiye wa mwaka 1 kwa mzozo na mkewe kuhusu 2K kodi ya nyumba

Kirinyaga: Mwanaume amuuwa bintiye baada ya kuzozana na mkewe kuhusu 2K za kulipa nyumba.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri13 April 2022 - 05:58

Muhtasari


• Mwanaume huyo walizozana na mkewe baada na mkewe huyo kumuomba pesa za kulipa kodi ya nyumba, kiasi cha shilingi elfu mbili.

Kisu cvha mauaji

Utafiti wa hivi karibuni unaonesha kwamba ongezeko la visa vya mauaji ya kinyumbani ni kutokana na ugumu wa maisha, unyongovu na msongo wa mawazo miongoni mwa Wakenya wengi ambao wanasukumwa na moja kati ya vyanzo hivyo hadi kufikia uamuzi wa kutekeleza mauaji ya watu wa karibu naye au hata kujiua wenyewe.

Usiku wa kuamkia Jumanne, mwanaume mmoja kutoka kaunti ya Kirinyaga alifanya kufuru ya mwaka baada ya kumuua bintiye mdogo kwa kile kilisemekana kwamba ni ugomvi wa nyumbani na mkewe, mamake marehemu.

Mwanaume huyo walizozana na mkewe baada na mkewe huyo kumuomba pesa za kulipa kodi ya nyumba, kiasi cha shilingi elfu mbili.

Hapo ndipo alicharuka juu na kughasiwa na mori ambapo alichukua kisu na kumdunga mara kadha bintiye wa mwaka mmoja unusu mpaka kufa baada yake kujaribu pia kujitoa uhai lakini akazuiliwa na watu waliowahi kufika katika eneo la tukio.

Alikimbizwa hospitalini na mwili wa mtoto huyo ukapelekwa katika cvhumba cha kuhifadhi maiti huku akisubiriwa kupona kabla ya kushtakiwa kwa kosa la mauaji na kujaribu kujiua pia.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved