logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanamke auawa kwa kudungwa kisu na 'landlord' South C, familia yalilia haki

Alidungwa kisu na kutupwa nje ya boma ambapo msanaria mwema alimkimbiza hospitalini.

image
na Radio Jambo

Habari25 November 2022 - 09:01

Muhtasari


• Marehemu alikuwa mama wa watoto watatu na mjane kufuatia kifo cha mumewe miaka mitatu iliyopita.

Crime scene

Familia moja inayoishi katika mtaa wa mabanda wa Kibera inalilia haki baada ya mpendwa wao kudaiwa kuuawa kwa kudungwa kisu na mwenye nyumba alikokuwa amekodisha kuishi.

Mwanamke huyo ambaye sasa ni marehemu kwa jina Anastacia Katumbi, 37, alidungwa kisu na mwenye nyumba mnamo Novemba 22 katika eneo la South C. Mwanamke ambaye ni mwenye nyumba katika eneo hilo alikuwa amempa kazi ya kusafisha na baada ya mzozano kiasi alimdunga kisu na kumuua.

Kulingana na Nation, Bi Katumbi alisaidiwa na mwanamke ambaye familia ilimtaja tu kama Mama Weru, ambaye alimkimbiza katika zahanati ya eneo hilo kabla ya kupelekwa katika Hospitali ya Mbagathi katika Kaunti Ndogo ya Lang’ata.

Mama Weru alisema kuwa alimuona mwanamke huyo akihangaika kwa maumivu, ndipo akaamua kumkimbiza hospitalini baada ya kutupwa nje ya boma hilo.

“Niliigiza tu nafasi ya msamaria mwema ambaye alikuwa amejitolea kuokoa maisha. Nimeambiwa kutoka huko alipelekwa katika Hospitali ya Mbagathi na baadaye akapewa rufaa ya Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta,” Nation ilimnukuu/.

Sasa imeibuka kuwa marehemu alikuwa mama wa watoto watatu na mjane kufuatia kifo cha mumewe miaka mitatu iliyopita.

Ana mtoto wa kwanza wa kiume, mwenye umri wa miaka 26, binti wa pili, mwenye umri wa miaka 22, na mzaliwa wake wa mwisho ana umri wa miaka 15.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved