logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Mimi ni mdogo sana kuenda jela!" Jambazi aliyependa aliyemuibia aiambia Korti

Aliiambia mahakama kuwa yeye bado ni mdogo na anahitaji msamaha kwani hataki kufungwa.

image
na Radio Jambo

Habari24 January 2023 - 09:04

Muhtasari


• Kipindi hicho akiwa na miaka 19, alivutiwa na msichana mmoja katika nyumba walimoiba na kuomba kubadilishana namba.

Mfungwa akiwa jela

Kijana mmoja aliyepatikana na hatia ya wizi wa kimabavu baada ya kumpenda mmoja wa wenye nyumba ambayo yeye na genge lake walifanya uvamizi, ameiomba mahakama kumpa msahama wa kutomfunga jela katika kile alisema kuwa yeye bado ni mdogo sana kufungwa.

Kevin Matundura mwenye umri wa miaka 24 pamoja na genge lake walivamia boma moja katika kaunti ya Nakuru mwaka 2017 lakini walipokuwa wanamaliza shughuli yao ya kuwaibia wenye nyumba, alivutiwa na kidosho mmoja kweney nyumba hiyo na kuomba wakabadilishane nambari za simu.

Baadae alianza kumtongoza kwa meseji za simu, jambo ambalo lilipelekea kukamatwa kwake pamoja na wenzake, baada ya polisi kutumia msichana huyo ili kumfikia mtuhumiwa.

Kesi yao imekuwa ikiendeshwa na mapema wiki jana, walipatikana na hatia ya wizi wa kimabavu ambapo walitarajiwa kuhukumiwa kifungo.

Lakini akijitetea mbele ya hakimu mkuu mkaazi wa mahakama ya Nakuru Jumatatu ya Januari 23 ambapo hukumu yao ilikuwa itolewe, Matundura alimuomba hakimu kumpa msamaha wa kutofungwa jela, akisema kuwa umri wake bado ni mdogo sana kuanza kuhudumia kifungo jela, huku akijutia kitendo chake.

“Niko katika umri mdogo na sitaki kukaa kizuizini maisha yangu yote. Nimepitia ushauri nasaha na ningependa niruhusiwe kurudi nyumbani na kurudisha kwa jamii,” alisema Matundura.

Katika kisa cha wizi kilichotokea usiku wa Machi 14, 2017, Matundura mwenye umri wa miaka 19 kipindi hicho na Wainaina walikuwa miongoni mwa genge la wanaume wanne waliovamia nyumba ya Bw James Wamugunda, mfanyabiashara na mkulima katika kaunti ndogo ya Bahati.

Hukumu hiyo iliyokuwa imepangwa Jumatatu ilikosa kufanyika baada ya mahakama kufahamishwa kuwa ripoti ya awali ya dhamana haikuwa tayari.

Mahakama iliahirisha hukumu hiyo hadi Februari 6.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved