logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Brian Mwenda aachiliwa kwa dhamana ya Ksh.200K

Alikanusha mashtaka yote mbele ya Hakimu Mkuu wa Nairobi Lukas Onyina.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri23 October 2023 - 14:37

Muhtasari


  • Katika kutoa dhamana, Hakimu Mkuu wa Milimani, Lukas Onyina, alisema upande wa mashtaka haukutoa sababu za msingi za kuwanyima dhamana mshtakiwa.
Wakili bandia Brian Mwenda.

Mahakama ya Nairobi imemwachilia anayedaiwa kuwa wakili feki Brian Mwenda kwa dhamana ya Ksh.200,000 pesa taslimu.

Katika kutoa dhamana, Hakimu Mkuu wa Milimani, Lukas Onyina, alisema upande wa mashtaka haukutoa sababu za msingi za kuwanyima dhamana mshtakiwa.

Mwenda wiki iliyopita alipandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka sita ya kutoa hati ya uongo, kutengeneza hati ya uongo pamoja na cheti cha kufanya kazi.

Alikanusha mashtaka yote mbele ya Hakimu Mkuu wa Nairobi Lukas Onyina.

Njagi alikamatwa na maafisa wa upelelezi wa DCI mnamo Oktoba 18 baada ya kufichuliwa kuwa wakili bandia.

Kesi hiyo itatajwa Novemba 7.

Upande wa mashtaka uliiomba mahakama kumnyima Mwenda dhamana kwa madai kuwa iwapo ataachiliwa hatahudhuria kesi mahakamani.

Mahakama pia iliambiwa kwamba mwenendo wa Mwenda unaonyesha kwamba hajali sheria, na kwamba alikwepa polisi kwa zaidi ya siku nne.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved