Alinur ashatkiwa kwa kuchapisha habari za uongo, aachiliwa kwa dhamana ya Ksh.30,000

Karatasi ya mashtaka inasema, "Mimi ni mwandishi wa habari niliyegeuzwa kuwa Msemaji wa ikulu

Muhtasari
  • Mahakama ilisikiliza maelezo hayo kwa uwongo yakimuonyesha Hussein Mohammed, MBS kama mwandishi akitumia akaunti ya X ya mtandao wa kijamii @Husseinmuhamedg, kwa nia ya kwamba data hiyo itachukuliwa kuwa ni ya kweli.
Image: DOUGLAS OKIDDY

Mwanasiasa Alinur Mohamed Bule ameshtakiwa kwa kuchapisha habari za uongo zinazodai kuwa yeye ni Msemaji wa Ikulu.

Bule alishtakiwa kuwa mnamo Julai 15 mwendo wa saa 1408 kwa kutumia akaunti yake ya X ya mtandao wa kijamii mahali pasipojulikana pamoja na watu wengine ambao hawakuwa mbele ya mahakama, alichapisha data za uongo kimakusudi.

Karatasi ya mashtaka inasema, "Mimi ni mwandishi wa habari niliyegeuzwa kuwa Msemaji wa ikulu, lakini siwezi kustahimili propaganda hii tena. Ni kinyume na maadili yangu kusema uwongo. Ni afadhali kupoteza kazi yangu kuliko kuhatarisha kanuni zangu."

Mahakama ilisikiliza maelezo hayo kwa uwongo yakimuonyesha Hussein Mohammed, MBS kama mwandishi akitumia akaunti ya X ya mtandao wa kijamii @Husseinmuhamedg, kwa nia ya kwamba data hiyo itachukuliwa kuwa ni ya kweli.

Alikanusha mashtaka mbele ya hakimu mkuu mwandamizi wa Milimani Robinson Ondieki.

Alinur aliwakilishwa na mawakili Sadam Hussein na Asha Bashir.

Aliachiliwa kwa dhamana ya pesa taslimu Sh30,000.

Kesi hiyo itatajwa Agosti 1.