logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jamaa afungwa jela miaka 4 kwa kumwacha mkewe nchini Sudan

Mwanamke huyo alihangaikia nchini Sudan kwa zaidi ya mwaka mmoja kabla ya kurudi Australia

image
na Brandon Asiema

Mahakama13 November 2024 - 15:05

Muhtasari


  • Mkewe mshukiwa aliishi nchini Sudan kwa takribani mwaka mmoja na miezi minne, kabla ya kupata usaidizi wa kisheria na uhamiaji kutoka kwa ubalozi wa Australia ulioko nchini Misri.
  • aji aliyesikiliza kesi hiyo Frank Gucciardo, alisema kwamba makosa aliyoyatekeleza jamaa huyo yalihusisha mipango ya makusudi kwani hakumtaarifu mkewe kuwa alikuwa ameondoa visa yake(mkewe) mnamo mwaka wa 2014.

caption

Mwanamume wa umri wa miaka 52 amefungwa jela miaka minne na nusu kwa makosa ya kumhada mkewe kuelekea nchini Sudan kisha kumwacha nchini humo akihangaika.


Mahakama moja nchini Australia imetoa hukumu hiyo baada ya kubaini kuwa mwanamume huyo alimlaghai mkewe kusafiri kuelekea Sudan kabla ya kuchukua watoto wake wawili pamoja na hati ya kusafiri ya mkewe na kurudi Australia.


Jaji aliyesikiliza kesi hiyo Frank Gucciardo, alisema kwamba makosa aliyoyatekeleza jamaa huyo yalihusisha mipango ya makusudi kwani hakumtaarifu mkewe kuwa alikuwa ameondoa visa yake(mkewe) mnamo mwaka wa 2014 jambo ambalo ikiwa mkewe angejaribu kuomba ombi ya kurejeshewa, ombi hilo lingekataliwa.


Jaji Frank alisema kwamba kitendo alichomfanyia mkewe kilikosa uungwana akiongeza kuwa mwanamke huyo alikuwa na huzuni mno wa kuondokewa kwa watoto wake.


Mkewe mshukiwa aliishi nchini Sudan kwa takribani mwaka mmoja na miezi minne, kabla ya kupata usaidizi wa kisheria na uhamiaji kutoka kwa ubalozi wa Australia ulioko nchini Misri.


Mwanamke huyo ambaye jina lake lilibanwa kwa sababu za kuisalama, alipata visa kutoka kwa wizara ya mambo ya ndani iliyomruhusu kusafiri hadi Australia mwishoni mwa mwezi Februari mwaka wa 2016.


Hata hivyo mwanamume huyo alikana shtaka dhidi yake la kumdanganya mkewe.


Aidha, wakati wa kusikilizwa kwa kesi hiyo kabla ya kutolewa kwa hukumu, mahakama hiyo ilielezwa na mke wa mwanamume huyo kwamba alikuwa na uzoefu mbaya sana kwani aliwahi kwama na watoto wake.

Katika barua iliyosomwa kortini, mkewe ambaye waliwachana alisema kuwa watoto wake walikuwa wamevumilia "mateso yasiyofikirika" baada ya kuondolewa bila idhini yake. Alisema kuwa mmoja wa watoto wake anakabiliwa na wasiwasi mkubwa wa kutengana na hadi sasa huwa  anahofia mama yake hatarudi anapoondoka.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved