logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jaji mkuu Martha Koome na majaji wenzake wa upeo wapata afueni

Mahakama kuu ya Narok ilitoa uamuzi wa muda kuzuia tume ya kuangazia mienendo na utendakazi wa Majaji JSC kutaka majibu ya majaji.

image
na Evans Omoto

Mahakama19 February 2025 - 15:57

Muhtasari


  • Jaji Charles Kariuki alipokuwa akitoa uamuzi wa kesi hiyo alitaja kesi hiyo kama ya dharura na kutoa uamuzi  wa kusitisha kwa muda mchakato wa kutaka majibu kwa wahusika waliotajwa kesini.
  • Akitoa uamuzi huo Jaji alieleza kuwa shinikizo la JSC kutaka majibu ya kesi  yao iliyowasilishwa dhidi ya majaji saba wa mahakama ya upeo ilikosa utaratibu maalum wa kuiendesha.

Afueni kwa Majaji wa mahakama ya upeo mahakama ya Narok ikisitisha kwa muda kesi ya JSC

Mahakama  kuu ya Narok ilitoa uamuzi wa muda kuzuia tume ya Huduma kwa mahakama JSC kutaka majibu ya mashitaka yaliokuwa  yamewasilisha kortini dhidi ya majaji wa mahakama ya upeo.

Uamuzi huo unatoa afueni ya muda   kwa Jaji mkuu Martha Koome,Naibu jaji mkuu Philomena Mwilu,Jaji Mohammed Ibrahim,Jaji Smokin Wanjala,Jaji Njoki Ndung’u ,Jaji Isaac Lenaola na Jaji William Ouko waliokuwa wakikabiliwa na vita vya kisheria kuhusu uwajibikaji na uhuru wao kikazi kama majaji.

Jaji Charles Kariuki alipokuwa akitoa uamuzi wa kesi hiyo alitaja kesi hiyo kama ya dharura na kutoa uamuzi  wa kusitisha kwa muda mchakato wa kutaka majibu kwa wahusika waliotajwa kesini.

Akitoa uamuzi huo Jaji alieleza kuwa shinikizo la JSC kutaka majibu ya kesi  yao iliyowasilishwa dhidi ya majaji saba wa mahakama ya upeo ilikosa utaratibu maalum wa kuiendesha.

Tume ya kuangazia utendakazi wa Majaji  JSC  ilikuwa imewasilisha kesi kortini mnamo Januari 27,2025 ikitaka majaji kujibu mashitaka  ya kesi nambari 35 ya 2024,72 ya 2024 na 3 ya 2025 mtawalia.

Mahakama hiyo ilitoa mwongzo kwa tume hiyo ya JSC ikitaka maelezo ya muongozo wa kisheria ambao JSC iliokuwa nao na iliokusudia kuutumia kuwaadhibu na kuwaadhibisha Majaji.

 Hata hivyo Korti ilisimamamisha mchakato huo wa JSC kutaka kuendelelea na Kesi hiyo hadi matakwa yote yatimie.

Hata hivyo mahakama ilitoa maelezo ikisema kuwa washitaki ni lazima wawasilishe majibu yao chini ya siku 21 baada ya uamuzi huo kutolewa na kila pande zote husika zipewe nyaraka husika ndani ya siku 14.

Kesi hiyo imeratibiwa kusikilizwa mnamo machi 12,2025 ili kudhibitisha iwapo maamuzi ya muongozo uliotolewa ka korti ulifutwa ipasavyo,gharama ya kusikilizwa kwa kesi hiyo itatolewa wakati wa mwisho wa kusikilizwa kwa kesi hiyo.

Itakumbukwa vyema kuwa siku chache zilizopita kulikuwa na shinikizo za mawakili wakishutumu uamuzi wa mahakama kuu uliotolewa wa kumzuia wakili Ahmednasir Abdullahi na kampuni yake dhidi ya kuendesha shughuli zozote za kisheria mahakani miongoni mwa madai mengini.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved