logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Pigo kwa Waititu kesi ya kuachiliwa kwa dhamana ikisongeshwa mbele mahakama yaamua

Ferdinand Waititu atasalia zaidi kwenye jela baada ya kesi aliyokuwa amewasilisha mahakamani akitaka kuachiliwa kwa dhamana kusongeshwa mbele.

image
na Japheth Nyongesa

Mahakama26 March 2025 - 12:20

Muhtasari


  • Waititu alikuwa amewasilisha kesi mahakamani akitaka mahakama kuu kumpa idhini ya kuachiliwa kwa dhamana.
  • Ombi hilo jipya lilikuja baada ya rufaa dhidi ya hukumu yake ya jela iliyowasilishwa na wakili wake ambayo bado inasubiri.
Former Kiambu governor Ferdinand Waititu and his wife Susan Wangari leave court earlier /EZEKIEL AMING’A

Waititu alikuwa amewasilisha kesi mahakamani akitaka mahakama kuu kumpa idhini ya kuachiliwa kwa dhamana jambo ambalo mahakama ya chini ilikuwa imepinga wakati wa kuamuliwa kwa kesi yake.

 Jaji wa Mahakama Kuu Lucy Njuguna aliamua kwamba Waititu anatalazimika kukaa kizuizini hadi Aprili 23 wakati mahakama itatoa uamuzi ikiwa inaweza kubadilisha rufaa yake.

Gavana huyo wa zamani Jumanne, Machi 18, aliwasilisha ombi jipya la kutaka kuachiliwa kwa dhamana huku akiendelea kutumikia kifungo jela baada ya kupatikana na hatia ya ufisadi.

Ombi hilo jipya lilikuja baada ya rufaa dhidi ya hukumu yake ya jela iliyowasilishwa na wakili wake ambayo bado inasubiri.

Waititu alitaka mahakama kumuachilia kwa dhamana wakati akingoja rufaa yake ambayo aliwasilisha isikilizwe na kuamuliwa. Gavana huyo wa zamani alifika mahakamani hii leo Jumatano 26 Machi kusikiliza hatima ya kesi yake ya kuachiliwa kwa dhamana.

 Waititu alizungukwa na kiongozi wa chama cha Wiper Kalonzo Musyoka na kiongozi wa Democratic Action Party-Kenya Eugene Wamalwa baada ya wao kufika mahakamani ili kukutana na yeye kama njia ya kuonyesha kumuunga mkono.

Mwanasiasa huyo  alikata rufaa yake ya kwanza  akiomba dhamana, ila mahakama ilikataa kumpa dhamana baada ya ombi lililofaulu la Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) kupinga ombi lake la kuachiliwa kwa dhamana.

Katika rufaa yake, Waititu alikuwa amesema afya yake ilikuwa mbaya, akilalamika kwa maumivu ya kifua na shinikizo la damu lakini yote haya yalionekana kuwa yasiyo na umuhimu. 

Duru zinaarifu kwamba mwanasiasa huyo maafufu aliondolewa katika jela ya viwandani [industral area prison] na kuhamishiwa jela ya kamiti.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved