logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Baba aliyeshtakiwa kufanya mapenzi na bintiye adai ni ishara ya upendo wa baba kwa bintiye!

Baada ya kuwafumania na kumkabili binti yake, alimwambia kwamba babake alimwambia anafanya naye mapenzi kama ishara ya upendo kwake kama mwanawe wa kumzaa.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Mahakama22 April 2025 - 11:43

Muhtasari


  • Alifunguka kwamba mumewe mwenye umri wa miaka 45 amekuwa akifanya mapenzi kisiri na binti yao mwenye miaka 19 katika kitanda chao cha ndoa.
  • Baada ya kuwafumania na kumkabili binti yake, alimwambia kwamba babake alimwambia anafanya naye mapenzi kama ishara ya upendo kwake kama mwanawe wa kumzaa.

Mahakama

MWANAMKE mwenye umri wa miaka 39 amesimulia mahakamani kwa majonzi jinsi aligundua mumewe amekuwa akifanya mapenzi na binti yao mwenye umri wa miaka 19.

Kwa mujibu wa mwanamke huyo aliyetoa ushahidi wake mbele ya hakimu, Alifunguka kwamba mumewe mwenye umri wa miaka 45 amekuwa akifanya mapenzi kisiri na binti yao mwenye miaka 19 katika kitanda chao cha ndoa.

Baada ya kuwafumania na kumkabili binti yake, alimwambia kwamba babake alimwambia anafanya naye mapenzi kama ishara ya upendo kwake kama mwanawe wa kumzaa.

Katika kesi hiyo iliyogonga vichwa vya habari jiji kuu la Zambia, Lusaka, BM, mwenye umri wa miaka 45  alikana mashtaka mawili ya kujamiiana na mashitaka mawili ya shambulio la aibu kwa wanawake kinyume na sheria za Zambia, jarida moja liliripoti.

Mshitakiwa huyo alifikishwa mbele ya Hakimu Mfawidhi Amy Masoja ambaye alimsomea mashitaka yote ambapo alikana kuyatenda.

Alipoitwa kwenye kizimbani cha shahidi kutoa ushahidi wake, BB, mke kwa mshtakiwa kwa zaidi ya miaka 23 na mama kwa mwathiriwa, alitoa ushahidi jinsi alivyogundua kuwa bintiye alikuwa akinyanyaswa na babake mzazi.

“Binti yangu MM alinieleza kuwa kati ya 2023 na 2024 kuna kitu kilimtokea, akaniambia baba yake anafanya kitu, nikamuuliza alikuwa anamfanya nini, akasema baba alikuwa akimshika matiti, nikamuuliza ni matiti tu ndiyo anaguswa akanyamaza.”

"Nilimwomba amalize kusema alichoanza jana usiku. Aliniambia kuwa siku nilipoenda kwenye Praise Overnight kwa Ushers na viongozi mwaka 2024, alisema alibaki na baba alifanya naye mapenzi," msichana huyo alisema.

BB alisema kitendo hicho kilitokea ndani ya nyumba, katika chumba kikuu cha kulala, chumba cha kulala cha wanandoa.

Mama wa manusura alisema binti huyo alipomkabili baba yake kwamba alichokuwa akifanya naye ni kibaya, mwanamume huyo alimwambia kuwa alikuwa akifanya naye mapenzi kwa sababu anampenda.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved