logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Papa John Paul II alikuwa anajua mapadre walawiti, lakini aliwaficha ripoti

John Paul alikuwa papa wa kanisa katoliki kutoka mwaka 1978 hadi 2005 alipofariki.

image
na Radio Jambo

Makala06 March 2023 - 06:15

Muhtasari


• Ripoti hiyo inaonesha wakati akiwa kadinali katika kanisa katoliki nchini Poland, alipokea malalamishi mengi ya ulawiti lakini hakuwachukulia hatua mapadre husika.

Papa John Paul wa pili

Aliyekuwa papa wa kanisa katoliki hayati John Paul alificha unyanyaswaji wa watoto kipindi akiwa kama papa, ripoti mpya imeonesha kulingana na majarida ya kitaifa.

Kulingana na ripoti moja iliyopeperushwa kwenye runinga ya TVN Jumapili jioni, Papa John Paul wa pili alikuwa anajua kuhusu unyanyasaji wa watoto katika kanisa la katoliki nyumbani kwao Poland lakini kipindi chote alificha hayo matukio.

Michal Gutowski, mpelelezi nyuma ya ufichuzi huo, alisema kwamba Karol Wojtyla, kama alivyokuwa akiitwa kabla ya kuwa Papa wakati huo, alijua kuhusu kesi za makasisi wanaolawiti watoto ndani ya kanisa alipokuwa bado kadinali huko Krakow. Aliwahamisha mapadre kwa dayosisi nyingine -- moja mbali kama Austria -- ili kuhakikisha hakuna kashfa yoyote iliyotokea, alisema, AFP walisema.

Wojtyla, ambaye alikuwa papa kwa miaka 27 kuanzia 1978 hadi kifo chake mwaka 2005, aliandika barua ya mapendekezo kwa kasisi anayetuhumiwa kwa unyanyasaji kwa kadinali wa Vienna Franz Koenig, bila kutaja shutuma hizo, anasema Gutowski kweney ripoti hiyo.

Wakati wa uchunguzi wake, mpelelezi huyo kwenye runinga alisema alizungumza na waathiriwa wa makasisi wanaolawiti watoto, familia zao na wafanyikazi wa zamani wa dayosisi ya kanisa.

Mpelelezio huyo kulingana na ripoti hiyo alisema kwamba kanisa lilimnyima idhini ya kufanyia uchunguzi nyaraka za marehemu John Paul.

Kanisa la Poland hapo awali lilikataa kutoa hati kwa mahakama au tume ya umma ya uchunguzi inayochunguza kesi za unyanyasaji wa watoto kanisani.

Waathirika kadhaa waliozungumza kwenye Makala hiyo na ambao hawakutana majina au sura zao kuweka wazi walikiri kutoa taarifa za makasisi waliokuwa wakiwalawiti watoto wavulana kwa papa John Paul lakini hakuwahi zingatia wala kuchukua hatua zozote za kinidhamu na kisheria.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved